-
Watu 33 wauawa katika hujuma ya anga ya Marekani nchini Syria
Mar 22, 2017 11:46Makumi ya raia wameuawa katika shambulio la anga la muungano wa kijeshi wa Marekani katika mkoa wa kaskazini wa Raqqah nchini Syria.
-
Asilimia 60 ya Waislamu Marekani wanabaguliwa
Mar 22, 2017 03:34Uchunguzi mpya wa maoni umebaini kuwa asilimia 60 ya Waislamu nchini Marekani wamebaguliwa kwa njia moja au nyingine katika kipindi cha mwaka moja uliopita.
-
Marekani kutuma zana mpya za kivita nchini Syria
Mar 22, 2017 03:05Marekani imeazimia kupeleka zana zake mpya za kivita nchini Syria sambamba na kutuma askari wengine 1,000 nchini humo.
-
Marekani na Uingereza zawabana zaidi wasafiri kutoka nchi kadhaa za Waislamu
Mar 22, 2017 02:58Serikali ya Marekani jana Jumanne ilipiga marufuku wasafiri kutoka nchi 8 za Waislamu kuingia katika ndege zinazoelekea nchini humo wakiwa na zana za electroniki kubwa zaidi ya simu za kiganjani. Nchi hizo 8 za Waislamu ni Jordan, Misri, Uturuki, Saudi Arabia, Kuwait, Morocco, Qatar na Imarati.
-
Luteka ya nchi za Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi kwa usimamiaji wa Marekani
Mar 21, 2017 10:27Luteka na mazoezi ya pamoja na kijeshi ya nchi za Kiarabu za Baraza la Ushirikiano wa Ghuba wa Uajemi yameanza nchini Kuwait kwa kushiriki vikosi vya nchi kavu vya nchi sita za Qatar, Kuwait, Imarati, Oman, Bahrain na Saudi Arabia.
-
Seneta Feinstein: Kuna uwezekano mkubwa Donald Trump atajiuzulu mwenyewe
Mar 21, 2017 10:05Seneta wa chama cha Democrat nchini Marekani amefichua kwamba, kuna uwezekano mkubwa Rais Donald Trump wa nchi hiyo atajiuzulu.
-
Licha ya upinzani wa Iraq, Trump asisitiza kubakia askari wa US nchini humo
Mar 21, 2017 04:15Licha ya pingamizi ya raia na viongozi wa Iraq juu ya kuendelea kuwepo askari wa kigeni ndani ya ardhi ya nchi yao, Rais Donald Trump wa Marekani amesisitizia kuwa askari wa nchi yake hawapaswi kuondoka nchini humo.
-
Safari ya Waziri Mkuu wa Iraq nchini Marekani; wasiwasi na matarajio yaliyopo
Mar 20, 2017 09:48Waziri Mkuu wa Iraq, Haidar al-Abadi, huku akiongoza ujumbe wa ngazi ya juu wa nchi yake jana alielekea mjini Washington kwa lengo la kufanya safari rasmi nchini Marekani.
-
Kupamba moto vita vya vyombo vya habari kati ya Russia na Marekani
Mar 20, 2017 04:48Bunge la Russia limeunga mkono pendekezo lililotolewa kuhusu kufanyika uchunguzi kuhusu vyombo vya habari vya Marekani vinavyofanya kazi huko Russia.
-
Utafiti: Vijana wengi Marekani wanasema Trump si rais halali
Mar 19, 2017 03:48Utafiti unaonyesha kuwa asilimia kubwa ya vijana wa Marekani wanamtazama Donald Trump kama rais ambaye si halali, mpuuzi na asiyekuwa na haiba ya uongozi.