-
Waziri Araghchi aanika nafasi ya Marekani, Israel katika ghasia za Iran
Jan 11, 2026 06:55Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi amezionya vikali Marekani na utawala haramu wa Israel juu ya matokeo mabaya ya uchochezi na uungaji mkono wao kwa wafanya fujo na wazua rabsha hapa nchini, akisisitiza kuwa Washington na Tel Aviv zinataka kuyageuza maandamano ya kiuchumi ya wananchi wa Iran kuwa machafuko na ghasia.
-
Waziri wa Ulinzi wa Pakistan: US ilipaswa kumteka Netanyahu, si Maduro
Jan 11, 2026 06:34Waziri wa Ulinzi wa Pakistan amesema "Marekani inapaswa kumteka nyara na kumshtaki katika mahakama yake yoyote ile Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel, Benjamin Netanyahu, ikiwa Washington ni rafiki halisi wa ubinadamu."
-
Kwa nini kunaibuka ufa baina ya Marekani na Ulaya?
Jan 11, 2026 02:29Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa amekosoa mwelekeo wa sera za kigeni za Marekani hivi sasa na kusema hivi sasa Marekani imeanza hatua kwa hatua kujiweka mbali na waitifaki wake sambamba na kukiuka sheria za kimataifa.
-
Marekani inahusika katika kugeuza maandamano ya amani kuwa machafuko nchini Iran
Jan 10, 2026 09:22Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Bw. Amir-Saeid Iravani katika Umoja wa Mataifa ameliandikia barua Baraza la Usalama la umoja huo akisema Marekani imeyageuza malalamiko na maandamano ya amani ya wananchi wa Iran kuwa ghasia na machafuko.
-
Ukosoaji mkali zaidi kuwahi kufanywa na Ujerumani: Marekani inaigeuza dunia "pango la wezi"
Jan 10, 2026 02:32Rais Frank-Walter Steinmeier wa Ujerumani amezikosoa vikali sera za nje za Rais wa Marekani Donald Trump na kuutaka ulimwengu usiruhusu nidhamu ya dunia ikageuzwa kuwa "pango la wezi".
-
Wazimu wa kijeshi wa Marekani; Bajeti ya kijeshi ya dola trilioni 1.5 kwa mwaka 2027
Jan 10, 2026 02:32Rais Donald Trump ametangaza kwamba anakusudia kuongeza bajeti ya kijeshi ya Marekani hadi dola trilioni 1.5 ifikapo mwaka 2027.
-
Marekani ina ndoto gani kuhusu mafuta ya Venezuela?
Jan 09, 2026 14:22Kufuatia operesheni ya kijeshi ya Marekani dhidi ya Venezuela, swali muhimu limeibuka: Washington ina mipango gani kwa ajili ya mafuta ya nchi hiyo?
-
Khatibu wa Sala ya Ijumaa: Waandamanaji watajitenga na wachache wanaovuruga amani
Jan 09, 2026 13:10Khatibu wa Sala ya Ijumaa ya leo ya mjini Tehran, Hujjatul Islam Sayyid Mohammad Hassan Abu Torabi Fard amesema, waandamanaji waelewa na wenye ghera ya uhuru na mamlaka imara ya nchi watatenganisha njia yao na ya wachache wanaoitakia mabaya nchi, wafanyao vitendo vya ukatili na kuvuruga nidhamu ya jamii; na hilo ni jambo lenye ulazima usioweza kuepukika.
-
Wacolombia waandamana kulaani vikali vitisho vya kijeshi vya Trump
Jan 08, 2026 12:42Maelfu ya wananchi wa wa Colombia wamefanya maandamano nchi nzima kulaani vitisho vya Rais Donald Trump wa Marekani dhidi ya nchi yao kama vile vya kuishambulia kijeshi Venezuela.
-
Wakazi wa Greenland: Tuna wasiwasi na mashinikizo ya Marekani kwa ajili ya kujimilikisha kisiwa hiki
Jan 08, 2026 12:36Wakazi wa kisiwa cha Greenland wameelezea wasiwasi wao kuhusu nia ya Marekani ya kujimilikisha kisiwa hicho kikubwa katika eneo la Aktiki, huku mijadala kuhusu mamlaka ya kujitawala ardhi hiyo ikipamba moto.