-
Kura ya veto ya Marekani dhidi ya azimio la Baraza la Usalama kuhusu vita vya Gaza
Dec 09, 2023 07:57Marekani, ambayo ni mwanachama wa kudumu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, imepinga azimio lililopendekezwa na UAE la kuanzisha usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza.
-
Barua isiyo ya kawaida ya Guterres kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya Gaza
Dec 07, 2023 08:28Katika hatua isiyo ya kawaida, Antonio Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametumia mamlaka aliyopewa kisheria kupitia kifungu cha 99 cha Hati ya Umoja wa Mataifa kulishinikiza Baraza la Usalama la umoja huo lianzishe haraka usitishaji vita huko katika Ukanda wa Gaza.
-
Waislamu Marekani waapa "kumdampu" Biden katika uchaguzi wa 2024 kwa sababu ya uungaji mkono wake kwa mauaji ya Israel
Dec 03, 2023 23:29Waislamu katika majimbo muhimu ya Marekani wamezindua kampeni ya #AbandonBiden kutokana na kukataa kwa rais huyo wa Merekani kutoa wito wa kusitishwa mashambulizi ya kinyama ya Israel huko Ukanda wa Gaza.
-
Kan'ani Chafi: Mashambulio mapya dhidi ya Gaza ni kashfa kubwa ya kimaadili kwa Marekani
Dec 02, 2023 23:45Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran ameandika katika kujibu idhini ya Marekani kwa mashambulizi mapya yanayofanywa na utawala wa Kizayuni dhidi ya wananchi wa Palestina katika Ukanda wa Gaza kwamba, hii ni kashfa kubwa ya kimaadili kwa serikali ya Marekani na imeonyesha sura halisi ya haki za binadamu ya Washington kwa walimwengu.
-
Iran: Wanyonyaji damu wa Kizayuni wameanzisha upya mauaji Gaza kwa uungaji mkono wa US
Dec 01, 2023 07:35Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema: baada ya kuwaua zaidi ya Wapalestina 15,000, wanyonyaji damu wa Kizayuni wameanzisha duru mpya ya mauaji huko Gaza kwa uungaji mkono kamili wanaoendelea kupewa na serikali ya Marekani.
-
Onyo la Moscow kuhusu kuendelea vita vya Ukraine mwaka 2024
Dec 01, 2023 04:29Licha ya kupita karibu miezi 22 tangu kuanza vita vya umwagaji damu nchini Ukraine, lakini hakuna matumaini yoyote yanayoashiria kumalizika mzozo huo hivi karibuni. Hii ni katika hali ambayo nchi za Magharibi kwa sasa zimeshughulishwa na vita vya Gaza na hivyo kutozingatia sana vita vya Ukraine, jambo ambalo limeipelekea serikali yenye mielekeo ya Kimagharibi ya Kyiv kukata tamaa kuhusu kupata misaada zaidi ya nchi hizo.
-
Russia yailaumu Marekani kwa mgogoro wa Gaza
Nov 30, 2023 00:22Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia amesema Marekani inapasa kubebeshwa dhima ya mgogoro baina ya Palestina na utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
-
Iran yazionya Marekani na Israel juu ya 'matokeo hasi makali' endapo jinai za kivita zitaendelea Gaza
Nov 28, 2023 09:52Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Hossein Amir-Abdollahian amezionya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel kwamba zitakabiliwa na "matokeo hasi makali" iwapo zitashindwa kukomesha kikamilifu uhalifu wa kivita katika Ukanda wa Gaza uliofanywa wakati wa vita vya mauaji ya halaiki dhidi ya eneo Palestina lililowekewa mzingiro.
-
Jeshi la Iran: Manowari ya Kimarekani yakubaliwa kuingia Ghuba ya Uajemi baada ya kujibu maswali yote ya Wanamaji wa Iran
Nov 28, 2023 04:14Kamanda wa Jeshi la Wanamaji la Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu IRGC amesema: Meli ya kubeba ndege za kivita ya Marekani ilikubaliwa kuingia Ghuba ya Uajemi kupitia Lango Bahari la Hormuz baada ya kujibu maswali yote ya vikosi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa lugha ya kifarsi.
-
Jeshi la Yemen laivurumishia makombora manowari ya US
Nov 27, 2023 07:16Kamandi Kuu ya Jeshi la Marekani katika eneo la Asia Magharibi (CENTCOM) limetangaza habari ya vikosi vya Jeshi la Yemen kuvurumisha makombora mawili ya balestiki na kulenga meli ya kivita ya Marekani ya 'USS Mason' katika Ghuba ya Aden.