-
Je, kwa nini Trump amenyamazia kimya mauaji ya kimbari huko Gaza, huku akidai yametokea Afrika Kusini?
May 23, 2025 05:57Akizungumza siku ya Jumatano katika kikao chenye mvutano na Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini, Rais Donald Trump wa Marekani alichukua hatua ya kushanga kwa kumuonyesha video ya kiongozi mmoja wa mrengo wa kulia wa Afrika Kusini aliyetoa wito wa kuuawa wakulima weupe ili kuthibitisha madai yake kuhusu kile kinachodaiwa kuwa mauaji ya kimbari dhidi ya wazungu wa nchi hiyo.
-
"Makubaliano na US yanaweza kufikiwa Washington ikiacha mashinikizo"
May 19, 2025 07:26Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian amesema mlango wa kufikia makubaliano na Marekani upo wazi iwapo Washington itaachana na tabia yake ya uonevu na sera zake za mashinikizo na kuiburuza Tehran katika mazungumzo kuhusu mpango wa nyuklia wa Jamhuri ya Kiislamu.
-
Mazungumzo yaliyogubikwa na mvutano mkubwa kati ya Trump na Zelensky
Mar 01, 2025 13:36Viongozi wenye mielekeo ya Kimagharibi wa Ukraine waliipa mgongo Russia baada ya matukio ya mwaka 2014 na kuingia madarakani serikali kibaraka kwa Magharibi huko Ukraine kwa himaya na msaada wa pande zote wa nchi za magharibi hususan Marekani na Ulaya; na walitaka nchi hiyo kujiunga na Muungano wa Kijeshi wa Nchi za Magharibi (NATO) na Umoja wa Ulaya (EU) na kukata uhusiano na Russia.
-
Waziri wa Mawasiliano wa Iran afanya mazungumzo na Rais wa Venezuela
Nov 05, 2024 07:15Katika siku ya kwanza ya ziara yake nchini Venezuela, Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Iran amekutana na kuzungumza na Rais wa Venezuela.
-
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu aonana na watungaji tungo za kishairi
Mar 26, 2024 02:56Jioni ya jana Jumatatu ambayo ilisadifiana na usiku wa mwezi 15 Ramadhani, siku ya kukumbuka alipozaliwa Imam Hassan al Mujtaba AS, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu alionana na jamii ya washairi na watu wa sanaa na utamaduni na kuzungumza nao kwa karibu na kwa mapenzi makubwa.
-
Mazungumzo ya Biden na Scholz: Kuongezeka mashinikizo dhidi ya Russia na misaada ya silaha kwa Ukraine
Mar 06, 2023 10:11Kitengo cha upashaji habari cha Ikulu ya Marekani, White House siku ya Ijumaa kilitoa taarifa baada ya mazungumzo ya rais wa nchi hiyo Joe Biden na kansela wa Ujerumani Olaf Scholz kikisema kuwa, nchi hizo mbili zimejipanga kuendelea na siasa za vvikwazo dhidi ya Russia hadi muda wowote zitakaohisi unafaa.
-
Mazungumzo ya Marais wa Iran na China; sisitizo la Xi Jinping juu ya umuhimu wa uhusiano wa pande mbili
Feb 16, 2023 02:26Jumanne ya juzi tarehe 14 Februari, Rais Ebrahim Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran alikutana na kufanya mazungumzo mjini Beijing na Rais Xin Jinping wa China.
-
Mtazamo wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu kuhusu dhulma za mfumo wa ubepari wa Magharibi kwa wanawake
Jan 05, 2023 05:31Ubepari wa Magharibi na demokrasia ya kiliberali, ambayo baada ya kuanguka kwa Umoja wa Kisovieti mnamo 1991, kulingana na wanafikra wengine wa Magharibi kama vile Francis Fukuyama, iliushinda mfumo wa kikomunisti kama mfumo bora wa kisiasa na kiuchumi, na kutambuliwa kama mwisho wa historia, sasa unakabiliwa na matatizo makubwa na ya kimsingi.
-
Mazungumzo ya Josep Borrell na Amir-Abdollahian nchini Jordan; msimamo baridi wa Umoja wa Ulaya
Dec 21, 2022 02:16Jumanne ya jana tarehe 20 Disemba, Waziri wa Mashauri ya Kiigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran alikutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya pambizoni mwa mkutano wa Baghdad-2 uliofanyika katika mji mkuu wa Jordan, Amman.
-
Sisitizo la Kiongozi Muadhamu kuwa mapambano ndio njia pekee ya kufikia ushindi dhidi ya Marekani
Jun 12, 2022 09:03Akizungumza jana Jumamosi alasiri katika kikao na Rais Nicolas Maduro wa Venezuela na ujumbe alioandamana nao, Ayatullah Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran amesisitiza juu ya kusimama imara Iran na Venezuela mbele ya mashinikizo makali na vita vya pande kadhaa vya Marekani na kusisitiza: Uzoefu wa mafanikio wa nchi mbili unaonyesha kwamba njia pekee ya kukabiliana na mashinikizo hayo ni mapambano na kusimamam imara.