Jul 23, 2018 13:49
Viongozi wa Saudi Arabia wamemzuia Sheikh Abd Al-Aziz Fawzan, mmoja wa mamufti wakubwa wa nchi hiyo, kutoka nje ya nchi na kadhalika kuendeleza shughuli zake katika mitandao ya kijamii kutokana na hatua yake ya kuukosoa utawala wa Aal-Saud juu ya vita vyake vya kichokozi nchini Yemen.