Apr 17, 2020 04:23
Katika kipindi hiki cha mgogoro wa mlipuko wa virusi vya corona, Marekani ambayo ni kinara wa nchi za Magharibi imeendeleza siasa zake zisizo za kibinadamu dhidi ya nchi hasimu na wapinzani wake, hususn katika kuzidisha vikwazo vya kiuchumi na kuzizuia kupata misaada ya kimataifa. Suala hili limekosolewa sana na madola mengine makubwa duniani.