Mratibu wa harakati inayopinga dhulma na ukandamizaji wa utawala wa Kizayuni Israel dhidi ya Wapalestina ametangaza kuwa, utawala wa Saudi Arabia unawashinikiza watu wa Palestina na kupalilia siasa za kibaguzi za Israel dhidi ya Wapalestina kwa hatua yake ya kuboresha uhusiano na utawala huo.
Msemaji wa Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina amesema kuwa, amani haiwezi kupatikana katika eneo la Mashariki ya Kati bila ya kuundwa nchi huru ya Palestina mji mkuu wake ukiwa Quds tukufu.
Rais Mahmoud Abbas wa Mamlaka ya Ndani yay Palestina amesisitiza kuwa, Beitul-Muqaddas ni mji mkuu wa abadi na milele wa Palestina.
Khatibu wa Msikiti wa al Aqsa amesisitiza kuwa, ulilmwengu unapaswa kufahamu kuwa, Quds Tukufu (Jerusalem) ni mji mkuu wa Palestina.
Viongozi wa kisiasa wa Palestina wametangaza kuwa, Intifadha ya Wapalestina itaendelea hadi pale rais wa Marekani atakapobatilisha uamuzi wake wa kuitambua Quds Tukufu kama mji mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel.
Wabunge wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran leo wamepitisha mpango wa dharura wa kuunga mkono Mapinduzi ya Kiislamu ya watu wa Palestina na kusisitiza kwamba Baitul Muqaddas utakuwa mji mkuu wa kudumu wa nchi ya Palestina.
Kiongozi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, Ismail Haniya amesema, mji wa Quds (Jerusalem) ulioungana ni mji mkuu wa nchi huru ya Palestina, na nchi za Kiislamu na Kiarabu hazitaipuuza Quds.
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Italia, Uingereza, Sweden na Ujerumani wamesema kuwa wana wasiwasi mkubwa na uamuzi wa upande mmoja wa Rais Donald Trump wa Marekani wa kuutambua rasmi mji wa Quds kama mji mkuu wa utawala wa Kizayuni.
Mkuu wa idara ya taifa ya afya nchini Angola amesema kuwa, watu 51 wamefariki dunia katika kipindi cha chini ya miezi mwili katika nchi hiyo ya kusini mwa Afrika kutokana na homa ya manjano.