Mar 13, 2022 02:24
Serikali ya Ethiopia ilisema jana Jumamosi kwamba itawachukulia hatua wahusika baada ya mkanda wa video kuonekana kwenye mitandao ya kijamii ukiwaonyesha watu wenye silaha, baadhi wakiwa wamevalia sare za kijeshi, wakiwachoma moto raia hadi kufa katika eneo la Magharibi mwa nchi hiyo.