-
Netanyahu na Lieberman wafutiwa kibali cha kuanzisha vita bila ya idhini ya baraza la mawaziri
May 24, 2018 22:49Baraza la Usalama la utawala wa Kizayuni wa Israel limebatilisha kibali alichokuwa amepewa waziri mkuu na waziri wa vita wa utawala huo cha kuanzisha vita dhidi ya nchi yoyote ile bila ya kupata idhini ya baraza la mawaziri.
-
Associated Press lafichua: Nentayahu alionana na mabalozi wa UAE na Bahrain, Washington
May 13, 2018 11:12Shirika la habari la Associated Press limefichua kuwa Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu alikutana na mabalozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na Bahrain nchini Marekani mnamo mwezi Machi mwaka huu, hatua inayozidi kuweka wazi uhusiano mzuri uliopo kati ya Israel na baadhi ya nchi za Kiarabu.
-
Malengo mawili ya makelele mapya ya Netanyahu dhidi ya Iran
May 04, 2018 02:20Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni, Jumatatu usiku aliendeleza vitendo vyake vya chuki na ghilba za kisiasa dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa kuonesha mbele ya kamera za vyombo vya habari vitu alivyodai kuwa eti ni ushahidi kwamba Iran inafanya juhudi za siri za kumiliki silaha za nyuklia.
-
Iran yaitaka Israel na waungaji mkono wake waache chokochoko zao la sivyo watajuta
May 01, 2018 23:17Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameuonya utawala haramu wa Israel na waungaji mkono wake na kuwataka waache njama na miamala yao hatari kwani jibu la Iran litakuwa la kushtukiza na la kuwafanya wajute.
-
Kuendelea madai ya kichekesho ya Netanyahu kuhusu Iran
May 01, 2018 02:48Waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel Jumatatu usiku, katika maonyesho yake mapya ya kipropaganda dhidi ya Iran, ameonyesha picha, CD na karatasi na kudai ni nyaraka zisizopingika kuhusu kile alichodai kuwa eti ni mpango wa siri wa Iran wa kuunda bomu la atomiki.
-
Mogherini ajibu mchezo wa kitoto wa Netanyahu kuhusu mapatano ya JCPOA
May 01, 2018 00:06Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya, usiku wa kuamkia leo amejibu mchezo wa kitoto wa Benjamin Netanyahu, waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel aliyedai kuwa eti Iran haijaheshimu mapatano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Haaretz: Iran; ajenda kuu ya mazungumzo ya Waziri mpya wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani na Netanyahu
Apr 29, 2018 03:19Gazeti la Kizayuni la Haaretz limeripoti kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni ajenda kuu itakayojadiliwa katika mazungumzo kati ya Mike Pompeo Waziri mpya wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani na Benjamin Netanyahu Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni.
-
Maelfu ya Waisraeli waandamana kupinga udikteta wa Netanyahu
Apr 22, 2018 09:13Maelfu ya Waisraeli wamemiminika mabarabarani kushiriki maandamano ya kupinga kile waliochokitaja kama udikteta wa Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni, Benjamin Netanyahu sambamba na kushinikiza afungwe jela kutokana na kashfa za ufisadi wa kifedha zinazomuandama.
-
Netanyahu afuta makubaliano na UN kuhusu wahajiri wa Kiafrika
Apr 03, 2018 21:59Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel amebatilisha makubaliano kati ya Tel Aviv na Umoja wa Mataifa, kuhusu kupelekwa katika nchi za Magharibi wahajiri wa Kiafrika wanaoishi katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na utawala huo ghasibu.
-
Erdoğan amwita Netanyahu 'gaidi' na aitaja Israel 'dola la kigaidi'
Apr 02, 2018 00:06Matamshi makali ya ukosoaji yaliyotolewa hivi karibuni na Rais Recep Tayyip Erdoğan wa Uturuki kuhusiana na jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina yamepelekea kuibuka vita vya maneno kati yake na Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel Benjamin Netanyahu.