-
Mahmoud Abbas: Marekani haisaidii juhudi za kurejesha amani Mashariki ya Kati
Aug 30, 2019 22:14Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina amesema kuwa Marekani haisaidii juhudi za kurejesha amani na usalama katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Makampuni ya Imarati yanunua ardhi za mji wa Quds kwa ajili ya Wazayuni
Aug 29, 2019 03:22Naibu Mwenyekiti wa Harakati ya Kiislamu ya Palestina amesema kuwa makampuni ya Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) yananunua ardhi huko Quds na kisha kukabidhi umiliki wa ardhi hizo kwa Waisraeli.
-
Arab League: Uamuzi wa Marekani wa kulifuta jina la Palestina ni kitendo cha "uadui"
Aug 28, 2019 22:07Jumuiya ya Nchi za Kiarabu (Arab League) imesema, uamuzi mpya uliochukuliwa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani wa kulifuta jina la Palestina katika orodha ya maeneo ya Magharibi ya Asia ni kitendo cha "uadui".
-
Marekani yafuta jina la Palestina katika orodha ya nchi za dunia
Aug 26, 2019 08:25Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imechukua hatua isiyo ya kawaida kwa kufuta jina la Palestina katika orodha ya nchi na maeneo mbalimbali ya dunia.
-
OIC: Baitul Muqaddas (Jerusalem) ni mji mkuu wa Palestina
Aug 22, 2019 07:41Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) imesisitiza kuwa: Baitul Muqaddas utabakia daima kuwa mji mkuu wa Palestina.
-
Wabunge Waislamu wa Marekani watamka hadharani kuwa iko siku ya karibu wataizuru Palestina ikiwa huru
Aug 18, 2019 22:13Wabunge wawili Waislamu katika Kongresi ya Marekani, ambao wamezuiwa kutembelea ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu wametangaza hadharani kuwa, iko siku ya karibu mno, wataitembelea Palestina ikiwa huru.
-
Utawala wa Kizayuni unashirikiana na Trump katika hatua dhidi ya wabunge Waislamu katika Kongresi ya Marekani
Aug 17, 2019 03:20Wizara ya Mambo ya Nje ya Utawala wa Kizayuni wa Israel imetangaza kuwa haitawaruhusu wajumbe wawili wa Bunge la Marekani, Kongresi, kuingia katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu.
-
Walowezi wa Kiyahudi wavamia Msikiti wa al Aqsa mara tatu siku ya Idi, wajeruhi makumi ya Waislamu
Aug 11, 2019 22:14Walowezii zaidi ya 1700 wa Kiyahudi jana walivamia Msikiti wa al Aqsa mara tatu katika siku ya Idul Adh'ha na kuwajeruhi makumi ya Waislamu waliokwenda eneo hilo takatifu kwa ajili ya kufanya ibada.
-
Saeb Erakat: Mamlaka ya Ndani ya Palestina inafuatilia kuundwa nchi ya Palestina
Aug 05, 2019 03:45Katibu wa kamati ya utendaji ya Harakati ya Ukombozi wa Palestina (PLO) ametangaza kuwa, mkakati wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina ni kuhitimishwa uvamizi na ukaliaji mabavu wa Wazayuni na kuundwa nchi ya Palestina.
-
Waziri Mkuu wa Palestina: Bila mfumo wa madola mawili, Israel itafikwa na kifo cha kidemografia
Jul 31, 2019 08:21Waziri Mkuu wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina Mohammad Shtayyeh amesema, utawala wa Kizayuni wa Israel utakabiliwa na "kifo cha kidemografia" ikiwa utakataa kuunga mkono suluhisho la kuwepo madola mawili, kwa ajili ya kutatua mgogoro wa miongo kadhaa baina yake na Wapalestina.