-
New York Times: Mgogoro wa Qatar umemshinda Trump
Sep 10, 2017 10:04Gazeti la New York Times la nchini Marekani limesema kuwa, rais wa nchi hiyo, Donald Trump ameshindwa kutatua mgogoro wa Qatar na nchi nne za Kiarabu zinazoongozwa na Saudia.
-
Kutokuweko viashiria chanya vya kutatuliwa mgogoro wa Qatar na kundi la 3+1
Sep 09, 2017 03:33Licha ya kuwa kumeanza duru mpya ya juhudi za upatanishi wa kuutatua mgogoro unaofukuta kati ya Qatar na kundi la 3+1, lakini Mohammed bin Abdulrahman Al Thani, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Qatar kwa mara nyingine tena amesisitiza kuwa, nchi yake itakaa katika meza ya mazungumzo pale tu mamlaka ya kujitawala Doha yatakapoheshimiwa na kutotiwa dosari.
-
Saudia yakubali kufanya mazungumzo na Qatar na kisha kughairi baada ya madakika
Sep 09, 2017 03:23Saudi Arabia imesimamisha mpango wa kufanya mazungumzo na Qatar kuhusu jinsi ya kuupatia ufumbuzi mgogoro kati ya Doha na nchi nne za Kiarabu zikiongozwa na utawala wa Riyadh, dakika chache baada ya kukubali kuja kwenye meza ya mazungumzo.
-
Qatar yashikilia msimamo wa kupinga masharti 13 ya Saudia ya kuanzisha tena uhusiano
Sep 08, 2017 03:12Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar, Mohammad bin Abdulrahman Aal Thani amesema, masharti 13 yaliyowekwa na tawala za Kiarabu zinazoongozwa na Saudia ambazo zimeiwekea nchi yake vikwazo, hayakubaliki kwani yanalenga kuhujumu mamlaka ya kijitawala Qatar.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar: Doha haiingilii masuala ya nchi yoyote
Sep 01, 2017 03:49Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar kwa mara nyingine tena amesisitiza kuwa Doha haiingilii masuala ya nchi yoyote na wakati huo huo hairuhusu nchi nyingine kuingilia masuala yake.
-
Somalia yakataa "rushwa" ya Saudia, yagoma kujiunga na nchi zinazoisusia Qatar
Aug 30, 2017 22:23Rais wa Somalia amekataa pendekezo la kupewa Euro milioni 68 lililotolewa na utawala wa Kifalme wa Saudi Arabia mkabala wa kujiunga na muungano wa nchi zilizokata uhusiano wao na kuisusia Qatar.
-
Mgogoro wa Riyadh na Doha wasababisha idadi ya Mahujaji wa Qatar kupungua
Aug 29, 2017 03:05Athari za mgogoro kati ya Doha na Riyadh zimeathiri pakubwa idadi ya Mahujaji wa Qatar walioenda kutekeleza ibada tukufu ya Hijja mwaka huu nchini Saudi Arabia.
-
Sisitizo la Qatar la kuimarisha uhusiano na Iran
Aug 24, 2017 08:54Wizara ya Mambo ya Nje ya Qatar imesema usiku wa kuamkia leo Alkhamisi kwamba Doha imeamua kumrejesha balozi wake mjini Tehran.
-
Senegal yapuuza ushawishi wa Saudia, sasa kumrejesha balozi wake nchini Qatar
Aug 22, 2017 03:43Serikali ya Senegal imetangaza kuwa, itamrejesha balozi wake ambaye awali ilimwita nyumbani baada ya kuanza mgogoro kati ya nchi za Kiarabu za eneo la Ghuba ya Uajemi na Qatar.
-
Qatar: Tunaishitaki Saudia kwa kutishia kushambulia ndege zetu za abiria
Aug 21, 2017 03:53Serikali ya Qatar imetangaza kuwa imekusudia kuishitaki Saudi Arabia katika Umoja wa Mataifa kutokana na nchi hiyo kutishia kuzishambulia ndege zake za abiria.