-
Balozi: Marekani inashajiisha vitendo vya kigaidi dhidi ya Russia
Jan 19, 2023 07:01Balozi wa Russia nchini Marekani ameonya vikali dhidi ya mashambulizi tarajiwa ya Ukraine katika Peninsula ya Crimea na kusisitiza kuwa, Moscow itajibu mapigo baada ya Washington kudokeza kuwa huenda Kiev ikatumia silaha za Magharibi kulishambulia eneo hilo.
-
Kuwasili nchini Iran kwa ndege za kivita aina ya Sukhoi 35, mapema mwaka ujao
Jan 15, 2023 03:36Mjumbe wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa na Sera za Kigeni ya Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) ameashiria kuwasili nchini mapema mwaka ujao wa Kiirani unaoanza Machi 21, ndege za kivita aina ya Sukhoi 35.
-
Russia: Waziri Mkuu wa Japan ni msaliti wa wahanga wa mashambulio ya nyuklia ya Marekani
Jan 14, 2023 22:53Naibu wa Mkuu wa Baraza la Usalama wa Taifa la Russia amesema kuwa, Waziri Mkuu wa Japan ni msaliti wa wahanga wa mashambulio ya nyuklia ya Marekani nchini mwake na kusisitiza kuwa, waziri mkuu huyo anatumikia malengo ya kibeberu ya Marekani.
-
Russia yadhibiti mji wa kistratajia wa Soledar, Donbass
Jan 14, 2023 00:20Wizara ya Ulinzi wa Russia imesema vikosi vya jeshi la nchi hiyo vimefanikiwa kudhibiti kikamilifu mji wa kistratajia wa Soledar, ulioko katika eneo la Donbass. Eneo la Donbass lenye raia wenye asili ya Russia liko mashariki mwa Ukraine na tangu 2014 Warusi walianzisha jamhuri mbili, Donetsk na Luhansk, na kuunda serikali zilizojitenga na serikali ya Ukraine.
-
Russia: Vikwazo vya Magharibi vimeshadidisha hali mbaya ya kibinadamu Syria
Jan 11, 2023 07:39Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Russia katika Umoja wa Mataifa amesema Wamagharibi wanabeba dhima ya kushtadi hali mbaya ya kibinadamu nchini Syria kutokana na vikwazo vyao vya upande mmoja.
-
Russia yaua askari 600 wa Ukraine katika shambulio la kulipiza kisasi
Jan 09, 2023 00:38Wizara ya Ulinzi ya Russia imetangaza kuwa, wanajeshi 600 wa Ukraine wameangamizwa katika shambulio la makombora la ulipizaji kisasi la Moscow katika eneo la Donbass.
-
UN yakaribisha usitishaji vita uliotekelezwa na Russia Ukraine
Jan 07, 2023 04:05Martin Griffiths, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayehusika na Masuala ya Kibinadamu, amesema usitishaji mapigano wa upande mmoja uliotekelezwa na Russia ni fursa ya kutuma misaada ya kibinadamu kwa watu katika maeneo yaliyoathiriwa na vita.
-
Russia yalalamikia vikao visivyoisha vya UN kuhusu faili la silaha za kemikali la Syria
Jan 06, 2023 23:08Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Russia katika Umoja wa Mataifa amelalamikia vikao visivyoisha na vya kila mwezi vya Baraza la Usalama la umoja huo kuhusu faili la silaha za kemikali la Syria na kusema kuwa, vikao hivyo vinafanyika kiudanganyifu kwa manufaa ya baadhi ya nchi za Magharibi.
-
Velayati: Uhusiano wa Iran na Russia ni wa kina, wa kimkakati na unaostawi
Jan 05, 2023 06:20Mshauri wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika masuala ya kimataifa amesema kwamba uhusiano wa Iran na Russia hivi sasa uko katika kiwango bora zaidi na unaendelea kustawi.
-
Putin atuma manowari yenye makombora ya hypersonic Bahari ya Atlantic, Hindi
Jan 05, 2023 03:44Rais Vladimir Putin wa Russia ameagiza kutumwa katika Bahari ya Atlantic na Bahari Hindi meli ya kivita iliyosheheni makombora ya hypersonic huku vita vya Ukraine vikipamba moto.