Jul 19, 2020 02:48
Siasa za kujichukulia hatua na maamuzi ya kipeke yake za Marekani katika miaka ya karibuni zimezusha hasira kali za viongozi wa nchi mbalimbali duniani; na aghalabu ya viongozi hao wamekosoa siasa hizo za Marekani na kusisitiza kutekelezwa siasa za ushirikiano wa pande kadhaa kwa maslahi ya pamoja. Katika msimamo wao wa karibuni wa kimataifa, Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Russia na China wamekosa kuendelea siasa hizo za kivyake vyake za Marekani katika masuala ya kimataifa.