-
Waziri wa Mambo ya Nje: Haijawahi kutokea mfano wa jinai za Saudia nchini Yemen
Mar 27, 2022 02:32Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Wokovu wa Kitaifa ya Yemen amesema kwa mnasaba wa kuingia mwaka wa nane wa vita vya kivamizi dhidi ya nchi yake kwamba, historia haijawahi kushuhudia mfano wa jinai za Saudi Arabia za nchini Yemen.
-
Makombora ya Yemen yateketeza kiwanda cha mafuta cha Aramco Jiddah, Imarati yatangaza hali ya hatari
Mar 26, 2022 08:07Wakati moto mkubwa ukiendelea kuteketeza kiwanda cha mafuta cha Aramco huko Jeddah nchini Saudi Arabia, kiwango cha tahadhari kimepandishwa juu katika Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kwa hofu ya operesheni za kijeshi za jeshi la Yemen na wapiganaji wa harakati ya Ansarullah wanaolipiza kisasi hujuma za muungano wa vita unaoongoza na Saudia.
-
Licha ya kuingia doa uhusiano wao, Marekani yaipatia Saudia mitambo ya kutungulia makombora
Mar 21, 2022 12:06Licha ya kuingia doa uhusiano wa Marekani na Saudi Arabia, afisa mmoja wa serikali ya Washington amesema, nchi yake imepeleka Saudia mitambo ya kutungulia makombora.
-
Sana'a yatoa masharti ili ikubali mwaliko wa PGCC wa kushiriki kikao cha Riyadh
Mar 17, 2022 22:45Waziri Mkuu wa serikali ya uokovu wa kitaifa ya Yemen ametangaza kuwa ili Yemen ikubali mwaliko wa Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi wa kushiriki katika kikao huko Riyadh; awali ya yote muungano vamizi dhidi ya Yemen unapasa kuchukua hatua tatu.
-
HRW yaitaka Saudi Arabia iwaachilie huru Wamisri 10 inaowashikilia
Mar 17, 2022 10:54Shirika la kimataifa la haki za binadamu la Human Rights Watch limeutaka ukoo wa Aal Saud unaotawala kiimla nchini Saudi Arabia uwaachilie huru Wamisri 10 inaowashikilia.
-
Jumuiya ya Kimataifa ya Mwamko wa Kiislamu: Kuna udharura wa kukabiliana na uhalifu wa Saudia
Mar 17, 2022 08:53Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Mwamko wa Kiislamu Duniani amelaani jinai ya Saudi Arabia ya kuwanyonga watu 81 na ametoa wito wa kuwepo umoja wa Waislamu na Ulimwengu wa Kiislamu kwa ajili ya kukabiliana na vitendo hivyo visivyo vya kibinadamu.
-
Safari ya Johnson Saudi Arabia; mafuta mhimili wa mazungumzo
Mar 16, 2022 07:15Wakati vita vya Russia na Ukraine vikiendelea na bei ya mafuta duniani kuendelea kupanda pia, Boris Johnson Waziri Mkuu wa Uingereza anaelekea Saudi Arabia kwa ajili ya kujadili suala la kupewa mafuta kwa bei rahisi.
-
Ayatullah Makarem Shirazi: Unyongaji wa umati wa Saudia umezijeruhi nyoyo za Waislamu wote huru
Mar 16, 2022 00:37Ayatullah Naser Makarem Shirazi, mmoja wa Marjaa Taqlidi wa mjini Qum nchini Iran amesema kuwa, hatua ya kuwanyonga makumi ya vijana Waislamu tena kwa sura ya kinyama na ya kikatili imezihunisha nyoyo za Waislamu wote huru ulimwenguni.
-
Kamishna Mkuu wa Haki za Kibinadamu wa UN alaani mauaji makubwa ya wafungwa Saudi Arabia
Mar 15, 2022 08:16Kamishna Mkuu wa Haki za Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa, Michelle Bachelet ametoa maoni yake kuhusu kunyongwa kwa watu 81 nchini Saudi Arabia.
-
Ansarullah ya Yemen imefanya operesheni kubwa ya mashambulio ndani kabisa ya ardhi ya Saudia
Mar 12, 2022 06:58Msemaji wa vikosi vya ulinzi vya Yemen ametoa ufafanuzi wa shambulio la ndege zisizo na rubani lililofanywa na jeshi la nchi hiyo ndani kabisa ya ardhi ya Saudi Arabia kujibu uchokozi na hujuma za kila leo wanazofanyiwa raia wa Yemen na muungano vamizi wa kijeshi unaoongozwa na utawala wa Riyadh.