-
Saudia imewanyonga watu 75 tangu ulipoanza mwaka huu
Mar 18, 2016 04:36Wizara ya Mambo ya ndani ya Saudia imetangaza kuwa imewanyonga watu wengine wawili ambao ni raia mmoja wa nchi hiyo na mwengine wa Yemen na hivyo kuifanya idadi ya watu waliouliwa kwa njia hiyo ya kunyongwa nchini Saudia tangu mwanzoni mwa mwaka huu kufikia 75.
-
Saudia kuwapiga kalamu nyekundu Wayemeni 35 elfu
Mar 15, 2016 23:27Saudi Arabia imesema kuwa karibuni hivi itawafuta kazi raia wa Yemen wapatao 35 elfu wanaofanya kazi nchini humo.
-
Hizbollah yalaani 'hujuma' ya Jumuiya ya nchi za Kiarabu
Mar 13, 2016 04:05Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Lebanon, Hizbullah, imelaani hatua ya hivi karibuni ya Jumuiya ya Nchi za Kiarabu kuitaja harakati hiyo kuwa "kundi la kigaidi" na kusema uamuzi huo ni sawa na "tangazo la hujuma" kutoka Saudi Arabia.
-
Amnesty: Huenda Saudia ikamnyonga mpwa wa Sheikh Nimr kesho!
Mar 12, 2016 11:55Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limeelezea hofu yake kuwa yumkini utawala wa Saudi Arabia hapo kesho ukamnyonga Ali Nimr, mpwa wa Shahidi Sheikh Nimr Baqir al-Nimr, mwanachuoni mkuu na maarufu wa Kiislamu aliyenyongwa na watawala wa Aal-Saud mapema mwaka huu.
-
Wasiwasi wa Umoja wa Mataifa kwa jinai za Saudia nchini Yemen
Mar 10, 2016 03:56Raia watatu wa Yemen wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa katika mashambulizi ya jana Jumatano ya ndege za muungano vamizi unaoongozwa na Saudi Arabia kwenye maeneo ya makazi ya raia katika mkoa wa al Jawf, kaskazini mwa Yemen.
-
Zarif: Saudia inachochea machafuko Mashariki ya Kati
Mar 06, 2016 03:49Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Mohammad Javad Zarif amesema Saudi Arabia inalenga kuchochea ghasia na machafuko Mashariki ya Kati.
-
Watoto elfu mbili wahanga wa uvamizi wa kijeshi wa Saudia Yemen
Mar 04, 2016 11:13Mratibu wa Oparesheni za Masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa watoto wasiopungua elfu mbili wameuawa na kujeruhiwa huko Yemen tangu Saudi Arabia ianzishe mashambulizi ya kijeshi nchini humo mwaka uliopita.
-
Kuendelea mapigano katika maeneo tofauti ya Yemen
Mar 04, 2016 02:11Licha ya Umoja wa Mataifa kuonya kuhusu hali mbaya ya kibinadamu nchini Yemen kutokana na mashambulio yanayofanywa na kundi linalojiita muungano wa Waarabu unaoongozwa na Saudia, mashambulio ya anga na mizinga ya kundi hilo yangali yanaendelea kwenye kona mbalimbali za Yemen.
-
Juhudi zilizofeli za Saudi Arabia huko Yemen
Mar 02, 2016 10:56Juhudi za jeshi la Saudi Arabia za kuukomboa mji wa al Rabia katika mkoa wa Asir kusini mwa nchi hiyo zimegonga mwamba hadi sasa.
-
Marekani, Israel, Saudia zinachochea fitna Mashariki ya Kati
Mar 01, 2016 23:20Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, Marekani, utawala wa Kizayuni wa Israel na Saudi Arabia zinachochea fitna na mizozo ya kimadhehebu katika eneo nyeti la Mashariki ya Kati.