-
US: Lengo la safari ya Trump Mashariki ya Kati ni dhidi ya Iran
May 15, 2017 03:05Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani amesema lengo kuu la safari ya wiki ijayo ya Rais Donald Trump wa nchi hiyo katika eneo la Mashariki ya Kati ni kwa ajili ya kuunda 'umoja' dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Mashambulizi ya Saudia nchini Yemen, yasababisha kuenea maradhi baina ya watoto
May 12, 2017 22:04Kuendelea vita na mzingiro wa kila upande unaofanywa na Saudi Arabia kupitia ndege za kivita za nchi hiyo huko Yemen, kumesababisha kuenea maradhi baina ya watoto wa taifa hilo masikini la Kiarabu, kiasi kwamba kila dakika 10 mtoto mmoja hufariki dunia kutokana na maradhi hayo.
-
Askari wa Saudia wavamia tena mashariki mwa nchi hiyo, waua na kujeruhi
May 11, 2017 00:13Wanaharakati wa Saudia wametangaza kwamba kwa mara nyingine tena askari wa utawala wa nchi hiyo wamevamia mji wa Al-Awamia ulioko eneo la Qatif katika mkoa wa Mashariki alikozaliwa Sheikh Nimr Baqir Nimr, mwanazuoni mkubwa aliyeuawa shahidi na utawala huo mwaka uliopita, na kusababisha maafa.
-
Iran yaionya Saudia dhidi ya kuchukua hatua yoyote ya kishenzi dhidi ya Tehran
May 08, 2017 02:26Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameuonya vikali utawala wa kifalme wa Aal-Saud dhidi ya kufanya maamuzi yoyote ya kipuuzi dhidi ya taifa hili na kusisitiza kwamba Jeshi la Iran halitachelewa kutoa jibu kali kwa kuusambaratisha utawala wote wa Riyadh.
-
Saudi yaipongeza Marekani kwa kuendeleza sera za uhasama dhidi ya Iran
May 06, 2017 09:19Adel al Jubeir, Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudi Arabia, katika safari yake ya hivi karibuni nchini Marekani, alizungumza na waandishi habari na kusema, safari ijayo ya rais Trump wa Marekani nchini Saudia itakuwa ya kihistoria huku akimpongeza rais huyo na serikali yake kwa misimamo yao mikali na ya uhasama dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Barua ya Iran kwa Umoja wa Mataifa; Saudi Arabia nembo ya ugaidi katika eneo
May 05, 2017 09:52Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa matamshi ya hivi karibuni ya Muhammad bin Salman, Naibu Mrithi wa Kiti cha Ufalme na Waziri wa Ulinzi wa Saudi Arabia dhidi ya Iran ni kinyume cha kipengee cha nne cha mada ya pili ya hati ya umoja huo na kwamba ni kukiri wazi nchi hiyo ya kifalme kuhusiana na uungaji mkono wake kwa vitendo vya mabavu na ugaidi.
-
Umoja wa Mataifa walaani siasa za ukandamizaji za utawala wa Saudia
May 05, 2017 03:00Ripota maalumu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Binadamu ameukosoa vikali utawala wa Saudi Arabia kwa kukiuka uhuru wa maoni, kuwatia nguvuni kiholela na kuwatesa wanaharakati wa kisiasa nchini humo.
-
Khoshrou: Matamshi ya Muhammad bin Salman, ni kitisho dhidi ya Iran na kukiri Saudia kuwa inahusika na ugaidi
May 05, 2017 00:08Mwakilishi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa, amesema kuwa matamshi ya hivi karibuni ya Kaimu Mrithi wa Kiti cha Ufalme na Waziri wa Ulinzi wa utawala wa kifalme wa Saudia, ni tishio dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu na ni kukiri kuwepo ushirikiano wa utawala wa Saudia na vitendo vya ukatili na ugaidi ndani ya Iran.
-
Saudia yaendeleza uhasama dhidi ya Iran, Muhammad Bin Salman adhihirisha chuki yake
May 03, 2017 00:07Naibu Mrithi wa Kiti cha Ufalme na Waziri wa Ulinzi wa utawala wa kifalme nchini Saudia, amebainisha chuki yake dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa kusema wazi kwamba, Saudia haitakuwa na mahusiano mazuri na Tehran.
-
Saudia imetumia fedha nyingi kuiziba mdomo jamii ya kimataifa isizungumzie jinai inazofanya Yemen
Apr 27, 2017 11:28Mkuu wa Taasisi iitwayo "Haki za Binaadamu kwa ajili ya Yemen" amesema kuwa, Saudi Arabia imetumia kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya kuinyamazisha jamii ya kimataifa isizungumzie jinai zake inazozitenda nchini Yemen na pia kuhusu hali mbaya ya kibinaadamu inayoshuhudiwa hivi sasa nchini humo.