-
UNESCO yasikitishwa na uchache wa urithi wa kihistoria barani Afrika ulioorodheshwa kwa shirika hilo + Sauti
Oct 02, 2018 06:58Wanahistoria na wasajili wa mambo ya kale wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamadunia (UNESCO) wamesikitishwa na uchache wa alama za kihistoria barani Afrika uliopo kwenye shirika hilo. Wataalamu hao ambao wametembelea Kigali nchini Rwanda wamesema kuwa asilimia 85 ya alama za kihistoria katika shirika hilo si za Afrika. Silvanus Karemera na ripoti kamili kutoka Kigali...
-
Waziri wa Mambo ya Ndani Tanzania: Watanzania wanaoishi mpakani wasisumbuliwe na vyombo vya usalama
Oct 01, 2018 01:37Waziri wa Mambo ya Ndani wa Tanzania, Alphaxard Kangi Ndege Lugola amevitaka vyombo vya ulinzi na usalama vya nchi hiyo kutowasumbua Watanzania wanaoishi mipakani lakini wakati huo huo wawatie mbaroni raia wa kigeni walioingia nchini humo kinyume cha sheria. Ammar Dachi ametuyarishia ripoti maalumu kuhusu suala hilo...
-
Burundi yashauriwa kujitoa katika Baraza la Haki za Binadamu la UN + Sauti
Sep 28, 2018 02:56Baada ya serikali ya Burundi kujiondoa kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC, mashirika yasiyo ya kiserikali nchini humo yameitaka serikali ya Bujumbura kujiondoa pia kwenye Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa.
-
Wanafunzi wenye ulemavu walalamikia changamoto zinazowakumba Zanzibar + Sauti
Sep 23, 2018 13:43Wanafunzi wenye ulemavu visiwani Zanzibar wamelalamikia changamoto wanazozipata wakati wanapokwenda mashuleni kutokana na kukosekana miundimbinu iliyo rafiki kwao. Mwandishi wetu Harith Subeit na ripoti kamili
-
Waziri Mkuu wa Tanzania aongoza maziko ya wahanga wa ajali ya MV Nyerere + Sauti
Sep 23, 2018 13:22Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa ameongoza mazishi ya kitaifa ya watu tisa kati ya 224 waliofariki kwenye ajali ya Kivuko cha MV Nyerere katika ziwa Victoria Septemba 20, 2018 ambao wamezikwa katika viwanja vya shule ya Sekondari Bwisya katika kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe mkoani Mwanza. Kati ya watu hao tisa, miili ya watu wanne ni ile ambayo haikutambuliwa. Mwandishi wetu wa Dar es Salaam Ammar Dachi anatutaarifu zaidi.
-
Mbatia: Ajali ya kuzama MV Nyerere nchini Tanzania ingeliweza kuepukwa + Sauti
Sep 22, 2018 03:05Mwenyekiti wa NCCR mageuzi nchini Tanzania, James Mbatia amesema kuwa, kuzama kivuko cha MV Nyerere katika ziwa Victoria ni ajali ya kujitakia.
-
Kagame akasirishwa na wanaosema amewaachilia huru wafungwa kwa mashinikizo
Sep 20, 2018 01:33Rais Paul Kagame wa Rwanda ameoneshwa kukasirishwa sana na wale wanaosema kuwa amewaachilia huru wafungwa kutokana na mashinikizo.
-
Serikali ya Uganda yautaka Umoja wa Ulaya usiingilie mambo yake ya ndani
Sep 17, 2018 12:45Serikali ya Uganda imeulalamikia vikali Umoja wa Ulaya na kuutaka uache tabia yake ya kuingia mambo ya ndani ya nchi hiyo ya Afrika Mashariki. Taarifa ya serikali ya Uganda imeeleza kuwa, umoja huo unapaswa kutambua kwamba, Uganda ni nchi huru na yenye kujiamulia mambo yake. Kwa taarifa zaidi na tumtegee sikio mwandishi wetu wa Kampala Kigozi Ismail….
-
Barabara ya juu ya Tazara jijini Dar es Salaam Tanzania kufunguliwa mwezi Oktoba 2018 + Sauti
Sep 16, 2018 13:27Ujenzi wa barabara ya juu katika eneo la Tazara jijini Dar es Salaam Tanzania umekamilika kwa asilimia 98 na unatarajiwa kufunguliwa mwezi Oktoba mwaka huu na Rais John Pombe Magufuli. Amari Dachi na maelezo zaidi...
-
Baraza la Seneti la Burundi kuchunga mashirika ya kigeni + Sauti
Sep 14, 2018 01:57Baraza la Seneti la Burundi lina mpango wa kuyachunguza mashrika ya kimataifa yanayotoa huduma nchini humo kubaini iwapo yanasajili wafanyakazi wake kwa kuzingatia usawa wa kikabila na kijinsia kama inavyoagiza sheria ya nchi hiyo au la. Mwandishi wetu Hamida Issa na ripoti kamili...