-
Ripoti: Waislamu, wahanga wakuu wa mashambulio ya al-Shabaab
Jan 17, 2020 04:06Uchunguzi uliofanywa na shirika moja lisilo la kiserikali umefichua kuwa, Waislamu ndio wahanga wakuu wa mashambulio ya kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab la Somalia, licha ya genge hilo kudai kuwa haliwalengi Waislamu na Wasomali katika hujuma zao.
-
UN: Mazungumzo ya amani Somalia ni ishara nzuri
Jan 09, 2020 21:05Mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia ambaye pia ni mkuu wa mpango wa umoja huo nchini humo UNSOM jana aliliutembelea mji wa Hargesa, makao makuu ya eneo lililojitangazia uhuru la Somaliland nchini Somalia na kukutana na viongozi wa eneo hilo kujadili uchaguzi na maendeleo.
-
Magaidi 33 wa kundi la al-Shabab waangamizwa nchini Somalia
Jan 04, 2020 10:04Wanamgambo wasiopungua 33 wa kundi la kigaidi la al-Shabab wameangamizwa katika operesheni mbili tofauti za jeshi kusini magharibi mwa Somalia.
-
Al-Qaeda yakiri kuhusika na shambulizi la bomu lililoua 90 Somalia
Dec 31, 2019 04:08Kundi la kigaidi la al-Shabaab lililojitangaza kuwa ni sehemu ya mtandao wa kigaidi wa al-Qaida limekiri kuhusika na shambulizi la bomu lililotokea mwishoni mwa wiki katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu na kuua makumi ya watu na kujeruhi wengine wengi.
-
Baraza la Usalama la UN lalaani mripuko wa Mogadishu, Somalia
Dec 30, 2019 23:15Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limelaani mripuko wa kigaidi uliotokea katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu na kuua makumi ya watu na kujeruhi wengine wengi.
-
Makumi wauawa katika mapigano ya kudhibiti kambi ya jeshi Somalia
Dec 24, 2019 08:40Makumi ya watu wameuawa katika makabiliano makali baina ya askari wa Jeshi la Taifa la Somalia na wanamgambo wa kundi la kigaidi la al-Shabaab karibu na mji wa Baidoa, kusini magharibi mwa Somalia.
-
Jeshi la Somalia lazima shambulizi la al Shabab dhidi ya Ikulu ya Rais mjini Mogadishu
Dec 11, 2019 03:21Jeshi la Somalia limetangaza kuwa, limewaangamiza wapiganaji 5 wa kundi la kigaidi la al Shabab waliojaribu kuingia na kuhujumu Ikulu ya Rais na hoteli moja iliyoko karibu na eneo hilo mjini Mogadishu.
-
Jubaland: Majeshi ya Ethiopia na Somalia yanataka kumpindua Rais Madobe
Nov 17, 2019 04:16Serikali ya eneo lenye mamlaka ya ndani la Jubaland, Kusini mwa Somalia imedai kuwa wanajeshi wa Ethiopia wanakula njama za kumpindua Rais Ahmed Madobe wa jimbo hilo.
-
OCHA: Mafuriko yameua watu 17 Somalia, 370,000 waachwa bila makazi
Nov 06, 2019 21:44Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Misaada ya Kibinadamu (OCHA) imesema watu wasiopungua 17 wameaga dunia baada ya kusombwa na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha nchini Somalia.
-
UN yatuma misaada kufuatia maafa ya mafuriko nchini Somalia
Nov 03, 2019 09:12Umoja wa Mataifa umetuma misaada ya dharura nchini Somalia kufuatia mvua kubwa ambazo zimenyesha katika baadhi ya maeneo ya nchi hiyo na kusababisha mafuriko.