-
Mwendesha Mashtaka Mkuu wa ICC: Najisikia aibu hatujafanya kazi nzuri huko Sudan
Sep 27, 2023 23:29Karim Khan, Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) amezungumza na televisheni ya France 24 pambizoni mwa Mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa huko New York akikiri kwamba taasisi hiyo haijafanya kazi nzuri kuhusiana na yanayojiri nchini Sudan.
-
OCHA: Mamilioni ya Wasudan wamekuwa wakimbizi kutokana na kuendelea vita na mapigano
Sep 23, 2023 23:45Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa mamilioni ya watu wamelazimika kuyahama makazi yao na kuwa wakimbizi kutokana na kuendelea vita na mapigano kati ya Jeshi na Vikosi vya Usaidizi wa Haraka, RSF nchini Sudan.
-
Ethiopia: Tumeanza duru mpya ya mazungumzo na Misri na Sudan kuhusu Bwawa Kuu la Renaissance
Sep 23, 2023 10:38Ethiopia imesema imeanza duru ya pili ya mazungumzo na Misri na Sudan kuhusu bwawa lenye utata lililojengwa na nchi hiyo kwenye mto Nile na kuwa chanzo cha mvutano wa muda mrefu kati ya mataifa hayo matatu.
-
Madhara ya kuendelea vita baina ya majenerali wa kijeshi nchini Sudan
Sep 23, 2023 02:54Licha ya kupita miezi mingi, lakini ndio kwanza vita baina ya majenerali wa kijeshi vinaendelea nchini Sudan na hali ya kisiasa na kiuchumi ya nchi hiyo inazidi kuwa mbaya siku baada ya siku. Cha kusikitisha ni kuwa pamoja na hali kuwa mbaya kiasi hicho, lakini bado pande hasimu zinaendelea kufanya ukaidi wa kutokubali kusimamisha mapigano.
-
Al-Burhan: Vita vya Sudan huenda vikaenea Afrika Mashariki
Sep 23, 2023 00:34Jenerali Abdul Fattah al-Burhan, mkuu wa baraza la uongozi la Sudan ameuonya Umoja wa Mataifa kuwa, vita vinavyoendelea kushuhudiwa katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika yumkini vitatanuka zaidi na kuenea katika nchi za Afrika Mashariki.
-
Mgogoro wa Sudan wajadiliwa kwa kina katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa
Sep 20, 2023 23:16Kandoni mwa Kikao cha 78 Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kumefanyika mkutano maalumu wa serikali na mashirika ya kimataifa ili kujadili mgogoro unaonedelea sasa nchini Sudan.
-
UN yashtushwa na vifo vya watoto katika kambi za wakimbizi Sudan
Sep 19, 2023 22:53Umoja wa Mataifa umesema watoto zaidi ya 1,200 wameaga dunia kutokana na ugonjwa wa surua na utapiamlo katika kambi za wakimbizi nchini Sudan.
-
Baraza Kuu la UN kujadili mgogoro wa Sudan kesho Jumatano
Sep 19, 2023 09:53Jumatano wiki hii Septemba 20, kutakuwa na kikao maalumu kandoni mwa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ili kukusanya misaada na kuonesha uungaji mkono kwa watu wa Sudan.
-
Mapigano makali yanaendelea katika mji mkuu wa Sudan, Khartoum
Sep 16, 2023 07:16Duru za habari nchini Sudan zimeripoti kuwa, mapigano makali yanaendelea kati ya vikosi vya Jeshi na Vikosi vya Usaidizi wa Haraka, RSF.
-
Vikosi vya RSF kuunda serikali katika maeneo vinavyoyadhibiti
Sep 15, 2023 08:32Vikosi vya Usaidizi wa Haraka vya Sudan (RSF) vimetishia kuunda mamlaka ya utawala katika maeneo yanayodhibitiwa na vikosi hivyo, iwapo 'maadui wao' wataunda serikali ya aina yoyote kwenye maeneo hayo.