-
UN: Wafanyakazi 82 wa ufikishaji misaada wameuliwa katika vita vya ndani Sudan Kusini
Apr 20, 2017 02:34Mratibu mkaazi wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini amesema wafanyakazi 82 wa utoaji misaada wameuliwa katika vita vya ndani vya nchi hiyo na kwamba idadi ya raia waliobaki bila makaazi sasa imefikia milioni tatu na nusu.
-
Indhari ya Unicef kuhusu kusimamia utoaji huduma huko Somalia na Sudan Kusini
Apr 19, 2017 02:58Mfuko wa Kuhudumia Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) umetahadharisha kuhusu kukosekana usimamizi wa utoaji huduma za kibinadamu kwa raia wa Sudan Kusini na Somalia.
-
Wimbi la mauaji laendelea Sudan Kusini, 14 wauawa
Apr 16, 2017 02:44Kwa akali watu 14 wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa katika mapigano mapya baina ya wanajeshi wa serikali na waasi katika mji wa Raga nchini Sudan Kusini.
-
WFP yalaani mauaji ya wafanyakazi wa ufikishaji misaada ya kibinadamu Sudan Kusini
Apr 14, 2017 22:00Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakuka Duniani (WFP) limelaani muaji ya wafanyakazi wake watatu wanaohudumu nchini Sudan Kusini.
-
Uingereza: Machafuko ya Sudan Kusini ni sawa na mauaji ya kimbari
Apr 14, 2017 03:48Waziri wa Serikali ya Uingereza amesema kuwa mauaji yaliyoyalenga makundi maalumu ya kikabila huko Sudan Kusini na kusababisha vita vya ndani nchini humo mwaka 2013, ni sawa na mauaji ya kimbari.
-
Watu 16 wauwa katika mapigano nchini Sudan Kusini
Apr 11, 2017 12:05Kwa akali watu 16 wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa katika mapigano baina ya wanajeshi wa serikali na waasi nchini Sudan Kusini.
-
Wakimbizi wa Sudan Kusini: Askari 'wamewachinja raia kama wanyama'
Apr 08, 2017 11:22Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) limesema watu zaidi ya 6,000 wamekimbia makazi yao nchini Sudan Kusini na kukimbilia wilaya ya kaskazini mwa Uganda ya Lamwo kujisalimisha na mauaji ya raia yanayofanywa na askari wa serikali ya Juba.
-
Wasi wasi wa Sudan kuhusu kuongezeka wimbi la wakimbizi wa Sudan Kusini
Apr 07, 2017 23:44Serikali ya Sudan imeonyesha wasi wasi wake mkubwa juu ya mgogoro unaotokana na ongezeko la wakimbizi wa Sudan Kusini wanaoingia nchi hiyo.
-
Jeshi na waasi Sudan Kusini watuhumiana kwa mauaji ya raia
Apr 05, 2017 11:36Msemaji wa Shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) ametangaza habari ya kukimbilia nchini Uganda maelfu ya raia wa Sudan Kusini kufuatia kushadidi mapigano ndani ya nchi hiyo changa zaidi barani Afrika.
-
Maafisa polisi zaidi ya 140 wa Rwanda wawasili nchini Sudan Kusini
Apr 05, 2017 03:13Rwanda imetuma makumi ya maafisa wa polisi wa kikosi kipya cha maafisa wake wa kulinda amani nchini Sudan Kusini.