-
Russia: Kuna ugumu katika utekelezaji wa makubaliano tuliyofikia na Uturuki kuhusu Syria
Oct 30, 2019 23:01Waziri wa Ulinzi wa Russia Sergey Shoygu amesema, utekelezaji wa makubaliano yaliyofikiwa hivi karibuni baina ya nchi yake na Uturuki kuhusu Syria umekuwa ukisuasua.
-
Kiongozi Muadhamu: Watu wa Iraq, Lebanon wafuatilie matakwa yao ya haki kwa njia za kisheria
Oct 30, 2019 08:32Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameashiria njama za maadui za kuvuruga usalama katika baadhi ya nchi za eneo na kusema: "Wanaojali Iraq na Lebanon wafahamu kuwa, kipaumbele chao kinapaswa kuwa kuondoa hali ya ukosefu wa usalama na wananchi wa nchi hizo nao wafahamu kuwa, matakwa yao ya haki yanaweza tu kukidhiwa katika fremu ya mfumo wa kisheria."
-
Marekani yatishia kukabiliana na Russia kijeshi kuhusu visima vya mafuta nchini Syria
Oct 30, 2019 00:58Wizara ya Ulinzi ya Marekani, Pentagon, imetishia kutumia nguvu za kijeshi dhidi ya yeyote atakayejaribu kuchukua visima vya mafuta inavyovidhiiti nchini Syria.
-
Wanajeshi wa Marekani warejea kaskazini mashariki mwa Syria
Oct 28, 2019 23:24Mamia ya wanajeshi wa Marekani ambao hivi karibuni waliondoka kaskaizni mwa Syria na kuelekea Iraq wamerejea katika kambi zao za awali huku wakiwa na zana chungu nzima.
-
Mousavi: Iraq na Syria ziliisambaratisha kitambo ISIS kwa msaada wa Iran
Oct 28, 2019 08:51Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh (ISIS) lilisambaratishwa na Iraq na Syria muda mrefu umepita, kwa msaada wa kilojistiki wa Jamhuri ya Kiislamu.
-
Picha za satalaiti zathibitisha; Marekani inafanya magendo ya mafuta ya Syria
Oct 26, 2019 08:53Russia imesema picha za satalaiti zimetoa ithibati kuwa Marekani inafanya magendo ya mafuta ya Syria chini ya ulinzi wa vikosi vyake vya usalama.
-
Trump aendelea kutoa misimamo ya nyuso mbili kuhusu Wakurdi wa Syria
Oct 25, 2019 03:40Rais wa Marekani kwa mara nyingine tena ametia ulimi puani na kubadilisha msimamo wake wa huko nyuma kuhusu Wakurdi wa Syria. Katika ujumbe wake mpya wa Twitter sasa Trump amewataka Wakurdi hao waende wakajikusanye kwenye maeneo yenye utajiri wa mafuta.
-
Rais Bashar al Assad atembelea mstari wa mbele wa vita dhidi ya magaidi kusini mwa Idlib
Oct 22, 2019 08:25Rais Bashar al Assad wa Syria akiwa pamoja na makamanda wa jeshi la nchi hiyo, amefika katika mstari wa mbele wa vita dhidi ya makundi ya kigaidi katika mkoa wa Idlib.
-
Marekani yasema iko tayari kutumia nguvu za kijeshi dhidi ya Uturuki
Oct 22, 2019 04:39Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani amesema Rais Donald Trump yuko tayari kutumia nguvu za kijeshi dhidi ya Uturuki iwapo 'italazimu'.
-
Mamia ya askari wa Marekani wanaoondolewa Syria kupelekwa Iraq
Oct 20, 2019 04:00Waziri wa Ulinzi wa Marekani amesema mamia ya wanajeshi wa nchi hiyo wanaoondolewa Syria watapelekwa nchini Iraq.