-
Maadhimisho ya Siku ya Ashura nchini Tanzania + Sauti
Sep 11, 2019 02:04Wakati Tanzania ikikaribia kufanya uchaguzi wa serikali za mitaa, viongozi wa dini mbalimbali wametakiwa kumuomba Mwenyezi Mungu ajaalie uchaguzi huo upite kwa salama na amani. Maelezo zaidi anayo mwandishi wetu wa Ammar Dachi...
-
Mahakama Tanzania yatupilia mbali ombi la Lissu la kupinga kuvuliwa ubunge; asema atadai haki yake Mahakama ya Rufaa
Sep 09, 2019 12:12Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Dar es Salaam imetupilia mbali maombi ya Mwanasheria Mkuu wa chama kikuu cha upinzani CHADEMA, Tundu Lissu ya kufungua shauri la kutengua uamuzi wa Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai uliosababisha kukoma kwa Ubunge wake Singida Mashariki.
-
Tanzania yaunga mkono juhudi za Afrika Kusini za kukomesha machafuko dhidi ya wageni + Sauti
Sep 05, 2019 11:31Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Profesa Palamaganda Kabudi, amesema kuwa serikali ya nchi hiyo ambayo hivi ni miongoni mwa nchi za SADC itakuwa bega kwa bega na serikali ya Afrika Kusini katika kuhakikisha machafuko yanayoendelea huko Afrika Kusini yanakomeshwa. Ammar Dachi na maelezo zaidi kutoka Dr es Salaam...
-
Mwito wa namna ya kuuadhimisha mwaka mpya wa Kiislamu + Sauti
Sep 02, 2019 05:10Waislamu nchini Tanzania wametakiwa kuukaribisha mwaka mpya wa Kiislamu kwa kukaa na kutathmini walichokifanya mwaka uliokwisha kwani kwisha kwa mwaka kuna maana ya kuzidi mwanadamu kuelekea kwenye siku yake ya kuondoka duniani. Ammar Dachi na maelezo zaidi kutoka Dar es Salaam...
-
Watanzania waandamana mbele ya ubalozi wa A. Kusini, wataka ndege ya ATCL irejeshwe
Aug 28, 2019 07:52Umati wa watu umeandamana leo nje ya ofisi za ubalozi wa Afrika Kusini jijini Dar es Salaam nchini Tanzania, wakishinikiza mahakama ya nchi hiyo iachie huru ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) inayoshikiliwa nchini Afrika Kusini kufuatia kesi ya fidia inayomhusu mtu ajulikanaye kama Hermanus Steyn wa nchi hiyo na Serikali ya Tanzania.
-
Tanzania kuwatimua wakimbizi wa Burundi, UNHCR yapinga
Aug 28, 2019 03:37Serikali ya Tanzania imetangaza kuwa wakimbizi wote kutoka nchi jirani ya Burundi watarudishwa makwao kuanzi Oktoba lakini Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNCHR limepinga hatua hiyo.
-
Sheikh Hemen Jalala alalamikia unyanyasaji wa Waislamu Tanzania + Sauti
Aug 26, 2019 02:25Mkuu wa chuo cha kiislamu cha Imam Swadiq AS kilichopo jijini Dar es Salaam Tanzania, Sheikh Hemed Jalala amesema kuwa kitendo cha kuwatilia shaka Waislamu wa kwa sababu ya kwenda nchi za Iran, Iraq, Syria, Saudi Arabia na Lebanon, ni kuvunja uhuru wao wa ibada. Ammar Dachi na maelezo zaidi...
-
Magari yanayotumia gesi yaongezeka nchini Tanzania
Aug 23, 2019 01:34Serikali ya Tanzania imebainisha kuwa matumizi ya gesi asilia katika magari yamezidi kukua nchini humo ambapo kwa sasa idadi ya magari hayo imefikia 210 kutoka 65 yaliyokuwa yakitumia nishati hiyo mwaka 2017. Mwandishi wetu Ammar Dachi ana maelezo zaidi kutoka Dar es Salaam....
-
Magufuli ahitimisha mkutano wa viongozi wa SADC, Dar
Aug 18, 2019 07:35Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ambaye ni Rais wa Tanzania, John Magufuli leo amefunga Mkutano wa 39 wa Jumuiya hiyo katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.
-
Mkutano wa SADC waanza Dar es Salaam
Aug 17, 2019 09:46Mkutano wa kilele wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) umeanza leo mjini Dar es Salaam nchini Tanzania.