-
WHO: Kesi 36 mpya za Ebola ziripotiwa DRC
Nov 30, 2018 01:03Hatari wa kuenea ugonjwa habari wa Ebola imeongezeka huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na katika nchi zinazopakana nayo baada ya kesi nyingine 36 kugunduliwa karibu na mpaka wa nchi hiyo katika wiki iliyomalizikia kwenye Novemba 29.
-
Magufuli: Wapinzani watulie la sivyo wataishia gerezani
Nov 27, 2018 11:40Rais John Magufuli wa Tanzania amempa ujumbe Waziri Mkuu wa zamani wa nchi hiyo Edward Lowasa awaambie viongozi wengine wa vyama vya upinzani kwamba watulie “la sivyo wataishia magerezani”.
-
ACT-Wazalendo yalaani uonevu kwa wavuvi Tanzania, naye Sheikh Ponda alilia katiba mpya
Nov 25, 2018 13:39Chama cha ACT- Wazalendo nchini Tanzania, kimelaani vikali vitendo vya ukiukwaji wa sheria na haki za binadamu vinavyofanywa dhidi ya wavuvi katika operesheni mbalimbali zinazotekelezwa nchini chini ya usimamizi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi.
-
Mbowe na Mbunge Ester Matiko wapelekwa mahabusu kwa muda usiojulikana nchini Tanzania
Nov 23, 2018 11:44Mahakama Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, Tanzania, imewafutia dhamana Mwenyekiti wa chama cha Chadema, Freeman Mbowe na Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Matiko kwa madai ya ukiukaji wa masharti ya dhamana, na kuanzia sasa watakuwa rumande hadi hapo kesi yao itakapomalizika.
-
Lema: Ni kosa kubwa kwa Benki Kuu ya Tanzania kuwatumia wanajeshi katika masuala ya kiraia
Nov 21, 2018 12:35Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani nchini Tanzania, ametupilia mbali hoja za Gavana wa Benki Kuu ya nchi hiyo, Profesa Florens Luoga kwamba, waliwatumia askari wa jeshi la wananchi (JWTZ) katika operesheni ya kulinda usalama wa maduka ya kubadilisha fedha, kwa kuwa kulikuwa na uhaba wa polisi.
-
Mufti wa Tanzania: Masheikh wa mikoa yote nchini endeleeni kukemea vitendo vya ushoga
Nov 20, 2018 12:04Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zuberi, amewataka masheikh na viongozi wa dini ya Kiislamu nchini humo kukemea vitendo vya ushoga.
-
Kenya yawakamata wavuvi 16 wa Tanzania kwa kuingia katika maji yake
Nov 19, 2018 00:46Polisi ya Kenya imewatia nguvuni wavuvi 16 raia wa Tanzania, kwa kuingia katika ardhi yake na kuvua samaki kinyume cha sheria.
-
Waislamu wahimizwa kusherehekea kwa amani na mapenzi Maulidi ya Mtume + Sauti
Nov 16, 2018 03:20Mkurugenzi wa Kitengo cha Utamaduni cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Tanzania Bw. Ali Bagheri amesema kuwa, maadhimisho ya Maulidi na kuzaliwa Mtume Muhammad SAW kunaleta mapenzi kwa Waislamu wote, hivyo waitumie fursa hiyo kuimarisha udugu wao. Amari Dachi na maelezo zaidi kutoka Dar es Salaam
-
Tanzania yazidi kubanwa, Denmark na Benki ya Dunia zaifutia ruzuku, mikopo
Nov 15, 2018 11:56Serikali ya Denmark imefuta mpango wake wa kuipa Tanzania msaada wa dola milioni 10 za Marekani, kulalamikia kile ilichotaja kama rekodi mbaya ya ukiukaji wa haki za binadamu nchini humo, na matamshi 'yasiyokubalika' dhidi ya mashoga.
-
Mufti wa Tanzania awahimiza Waislamu kujifunza sayansi + Sauti
Nov 11, 2018 14:03Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakari Zuberi bin Ali amewataka Waislamu wa Tanzania kujiendeleza na kujitanua katika nyanja mbalimbali za kielimu hasa katika sekta ya sayansi na teknologia ili kuiendeleza dini ya Kiislamu kwa njia bora zaidi. Ammari Dachi na taarifa zaidi kutoka Dar es Salaam...