-
Corbyn: Trump ni mbaguzi, Uingereza haipaswi kumtandikia 'zulia jekundu'
Apr 27, 2019 03:10Kiongozi wa chama Leba nchini Uingereza amekosoa vikali mpango wa nchi hiyo wa kumpa mapokezi ya hali ya juu Rais Donald Trump atakapoitembelea nchini hiyo mwezi Juni mwaka huu, akisisitiza kuwa rais huyo wa Marekani ni mbaguzi na mtu mwenye hulka ya kuwadhalilisha na kuwatweza wanawake.
-
Bunge la Uingereza latahadharisha juu ya uwezekano wa kutokea vita vya silaha za nyuklia duniani
Apr 26, 2019 02:08Kamati ya Mahusiano ya Kimataifa ya Bunge la Uingereza imetoa taarifa inayoonya juu ya uwezekano wa kutokea vita vya silaha za nyuklia kati ya nchi zenye silaha hizo.
-
Upinzani: Uingereza haipaswi kumkabidhi Julian Asange kwa Marekani
Apr 12, 2019 10:27Kiongozi wa chama Leba nchini Uingereza amekosoa vikali kitendo cha kutiwa mbaroni mjini London mwasisi wa mtandao unaojishughulisha na kufichua siri na kashfa wa WikiLeaks, Julian Assange.
-
Maandamano yashuhudiwa London baada ya kukamatwa mwasisi wa Wikileaks
Apr 11, 2019 23:59Maandamano yameshuhudiwa nje ya ubalozi wa Ecuador mjini London baada ya polisi ya Uingereza kumtia mbaroni mwasisi wa mtandao unaofichua fedheha nyingi za nchi na viongozi mbalimbali duniani wa WikiLeaks, Julian Assange, ambaye amekuwa akiishi ubalozini hapo tokea mwaka 2012.
-
Mamia waandamana London, Uingereza dhidi ya utawala haramu wa Israel
Mar 30, 2019 22:42Mamia ya watu wamejitokeza katika barabara za London, mji mkuu wa Uingereza kushiriki maandamano dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Makomandoo wa Uingereza wajeruhiwa na vikosi vya Yemen
Mar 24, 2019 03:27Duru mpya za habari zimefichua kuwa, makomandoo kadhaa wa Uingereza wamejeruhiwa katika makabiliano ya ana kwa ana na vikosi vya Yemen, na hivyo kuweka bayana kuwa serikali ya London imekuwa ikishiriki moja kwa moja katika vita vya muungano vamizi wa kijeshi unaoongozwa na Saudia dhidi ya nchi hiyo maskini ya Kiarabu.
-
Waingereza waandamana London kutaka kufanyika kura mpya ya maoni kuhusu Brexit
Mar 24, 2019 03:01Mamia ya maelfu ya wananchi wa Uingereza wamefanya maandamano katika mji mkuu London, kushinikiza kufanyika kura mpya ya maoni kuhusu suala la kujitoa nchi hiyo katika Umoja wa Ulaya (Brexit).
-
Misikiti mitano yavamiwa katika mji wa Birmingham nchini Uingereza
Mar 21, 2019 11:34Misikiti mitano imeshambuliwa katika mji wa Birmingham nchini Uingereza, wiki moja baada ya kutokea mashambulizi ya kigaidi nchini New Zealand na kuua makumi ya Waislamu na kujeruhi makumi ya wengine.
-
Waasi wanaotaka kujitenga Ireland wakiri kutuma mabomu London
Mar 12, 2019 22:55Kundi la waasi la Irish Republican Army (IRA), ambalo linataka eneo la Ireland ya Kaskazini lijitenge na Uingereza limekiri kuhusika na utumaji wa vifurushi vya mabomu katika mji mkuu wa Uingereza, London na Scotland.
-
Wazazi wawarejesha vijana wao Somalia ili wasichomwe visu Uingereza
Mar 10, 2019 23:08Kutokana na kushtadi hujuma za visu nchini Uingereza, wazazi wa Kisomali wamewarejesha kwa wingi vijana wao nchini Somalia.