-
Kushtakiwa Ujerumani katika Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu (ICJ) kwa kuiuzia silaha Saudia
Dec 18, 2019 23:01Kuendelea vita vya Yemen na kuuawa maelfu ya raia wa nchi hiyo katika vita hivyo, kumezipelekea baadhi ya asasi na mashirika ya haki za binaadamu kukosoa vikali siasa mbovu na hatua za nchi za Ulaya ikiwemo ya kuuzia silaha muungano vamizi wa Saudia unaoongoza vita hivyo dhidi ya Yemen.
-
Nchi za Magharibi zinatumia vibaya suala la haki za binadamu kwa kisingizio cha kutetea watu
Dec 13, 2019 23:32Abbas Musawi, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, amelaani msimamo wa hivi karibuni wa Heiko Maas, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani wa kutumia kisiasa matukio na ghasia za hivi karibuni nchini Iran.
-
Mousavi: Matamshi ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani yanangilia mambo ya ndani ya Iran
Dec 13, 2019 09:21Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imejibu matamshi yaliyotolewa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani akisema kuwa matamshi kama hayo yanayoingilia masuala ya ndani ya Iran hayaweza kuficha makosa ya baadhi ya nchi za Ulaya ya kutotekeleza majukumu yao katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA na misimamo yao isiyo sawa kuhusiana na ugaidi wa kiuchumi wa Marekani.
-
Watu wenye chuki watishia kulipua kwa bomu msikiti mjini Berlin, Ujerumani
Nov 26, 2019 01:09Viongozi wa msikiti wa Sehitlik mjini Berlin, mji mkuu wa Ujerumani wametangaza kwamba watu wenye chuki dhidi ya dini ya Uislamu miongoni mwa makundi ya mrengo wa kulia na yenye misimamo ya kigaidi, wametishia kulipua kwa bomu msikiti huo.
-
Indhari ya Mshauri wa Usalama wa Taifa Marekani kuhusu kusambaratika NATO
Nov 12, 2019 04:27Rais Donald Trump wa Marekani ambaye ni maarufu kwa kuibua utata, angali anaendelea kukosoa vikali Muungano wa Kijeshi wa Atlantiki ya Kaskazini (NATO) . Trump hasa anawakosoa wanachama wa bara Ulaya katika muungano huo kwa kutotenga asilimia 2 ya Pato la Ndani la Nchi (GDP) kwa ajili ya gharama za kijeshi. Maafisa wa ngazi za juu wa Marekani nao sasa pia wanafuata nyayo za Trump katika kuukosoa muungano wa kijeshi wa NATO.
-
Rais wa Ujerumani akosoa sera za kijuba za Marekani
Nov 11, 2019 03:35Siasa za kijuba na misimamo inayokiuka sheria za kimataifa ya Marekani imekuwa ikipingwa na kukosolewa na nchi nyingi duniani na hata washirika wa nchi hiyo barani Ulaya.
-
Taarifa ya pamoja ya Kansela wa Ujerumani na Waziri Mkuu wa India kuhusu makubaliano ya JCPOA
Nov 03, 2019 04:21Makubaliano ya nyuklia ya Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA) ambayo yalikuwa natija ya juhudi za kidiplomasia na mazungumzo ya awamu kadhaa kati ya Iran na kundi la 5+1; hivi sasa yanakabiliwa na hatari kubwa kufuatia hatua ya Marekani ya kujitoa kwenye makubaliano hayo na kutotekeleza ahadi nchi za Ulaya; hatua iliyokabiliwa na radiamali kali ya Iran ambayo pia imeamua kupunguza hatua kwa hatua uwajibikaji wake ndani ya makubaliano hayo.
-
Ujerumani: Hatukubali kufanywa wenzo wa kutekeleza siasa za Marekani dhidi ya Iran
Sep 25, 2019 04:18Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani sambamba na kuashiria kuwa nchi yake ni nchi huru inayojiamulia yenyewe mambo yake amesema kuwa, Berlin haiko tayari kuwa sehemu ya wenzo wa Marekani ya kutekeleza siasa zake za vikwazo vya kiwango cha juu kupindukia dhidi ya Iran.
-
Ujerumani yarefusha kwa miezi sita mingine marufuku ya silaha kwa Saudia
Sep 19, 2019 02:42Serikali ya Angela Merkel imeongeza kwa miezi mingine sita marufuku ya silaha zote za Ujerumani inazoziuzia Saudi Arabia licha ya miito inayotaka kulegezwa marufuku hiyo.
-
'Kushambuliwa vituo vya mafuta vya Saudia, kunabainisha udhaifu na kushindwa kwa Riyadh'
Sep 17, 2019 07:55Mtaalamu na mchambuzi wa masuala ya Magharibi mwa Asia amekadhibisha madai yaliyotolewa kwamba Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imehusika katika shambulizi dhidi ya taasisi za mafuta za Saudi Arabia na kusema kuwa, shambulizi hilo kwenye taasisi hizo limeonyesha udhaifu na kushindwa kwa Wasaudi.