-
Njama za Magharibi za kuanzisha NATO ya dunia nzima
May 18, 2022 09:28Katika hali ambayo suala la uwanachama wa nchi mbalimbali hasa Ukraine katika Jeshi la Nchi za Magharibi NATO limeitumbukiza dunia kwenye mgogoro wa kimataifa, Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza ameona kama hiyo haitoshi na hivi sasa amezungumzia wajibu wa kuweko mkataba wa NATO ya dunia nzima.
-
Putin atia saini amri ya kuiwekea vikwazo vya ulipizaji kisasi kambi ya Magharibi
May 05, 2022 02:15Ikulu ya Kremlin imetangaza Jumanne kuwa, Rais Vladimir Putin wa Russia ametia saini amri ya kukabiliana na 'hatua zisizo za kirafiki za baadhi ya nchi za kigeni na mashirika ya kimataifa." Dikrii hiyo inasisitiza hatua za kulipiza kisasi dhidi ya nchi ambazo zimetajwa kuwa 'zisizo za kirafiki'. Kwa mujibu wa amri hiyo Russia itaziwekea vikwazo baadhi ya nchi na taasisi za kimataifa.
-
Russia yawakatia gesi Wapoland, sarafu za Euro na Pound ya Uingereza zaporomoka
Apr 28, 2022 02:49Sarafu za Euro na Pound ya Uingereza zimeporomoka thamani yake baada ya Russia kuamua kuzikatia gesi nchi za Poland na Bulgaria kutokana na kufuata kwao kibubusa siasa za Magharibi.
-
Kuongezeka vitendo vya chuki dhidi ya Uislamu barani Ulaya na vigezo vya undumakuwili kuhusu uhuru wa kujieleza
Apr 18, 2022 11:13Mwenendo wa chuki dhidi ya Uislamu na vitendo vya mabavu dhidi ya Waislamu vimeongezeka katika miaka ya karibuni katika nchi za Ulaya. Kujitokeza na kuongezeka kwa harakati, vyama na watu wenye misimamo mikali wa mrengo wa kulia kumekuwa na nafasi kuu katika uwanja huo.
-
Shirika la Afya Duniani linakosoa kuondolewa vizuizi vya corona barani Ulaya
Mar 23, 2022 11:46Shirika la Afya Duniani (WHO) limekosoa hatua ya kuondolewa vikwazo vya corona katika nchi za Ulaya.
-
Kuongezeka propaganda za kueneza chuki dhidi ya Russia barani Ulaya
Mar 09, 2022 08:08Huku mgogoro ukizidi kuwa mkubwa baina ya Russia na nchi za Magharibi hususan kutokana na kupamba moto mapigano nchini Ukraine, mashinikizo yanayotokana na vikwazo vya Magharibi dhidi ya Russia nayo yameongezeka.
-
Raia wa Russia wakwama na kutangatanga katika viwanja vya ndege vya nchi za Ulaya
Mar 02, 2022 03:36Vyombo vya habari vya Russia vimetangaza kuwa, raia wa nchi hiyo wanatangatanga katika viwanja vya ndege vya nchi za Ulaya kufuatia uamuzi wa Umoja wa Ulaya kuiwekea Russia vikwazo vya anga.
-
Russia: Hatutaki vita barani Ulaya wala Ukraine
Feb 16, 2022 07:10Rais wa Russia amesema kuwa nchi yake haitaki kutokee vita barani Ulaya wala nchini Ukraine na ni kwa sababu hiyo ndio maana imetoa pendekezo la kudhaminiwa usalama wa eneo hilo.
-
Kuongezeka indhari kuhusu uwezekano wa kutokea vita mashariki mwa Ulaya
Feb 12, 2022 10:13Nchi za Magharibi zinaendelea kutoa tahadhari mbalimbali kuhusu uwezekano wa Russia kuishambulia Ukraine kufuatia kuongezeka mivutano huko Ulaya Mashariki kati ya Moscow na Kiev.
-
Nchi nne za Ulaya zataka kusimamishwa ujenzi wa vitongoji vya Wazayuni katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu
Jan 20, 2022 10:37Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi nne za Ulaya ambazo ni Ufaransa, Ujerumani, Italia na Hispania wamesema kuwa uamuzi wa viongozi wa utawala haramu wa Israel wa kujenga vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika ardhi za Wapalestina zinazokaliwa kwa mabavu na utawala huo ni ukiukaji wa wazi wa sheria za kimataifa.