-
OCHA: Misaada zaidi ya kibinaadamu inahitajika kwa ajili ya Waislamu wa Myanmar
Sep 22, 2017 01:02Ofisi ya Uratibu ya Umoja wa Mataifa Inayoshughulikia Masuala ya Kibinaadamu (OCHA) imetoa mwito wa kuongezwa bajeti ya misaada ya kibinaadamu kwa ajili ya wakimbizi Waislamu wa kabila la Rohingya wa nchini Myanmar.
-
Rais Hassan Rouhani atoa hotuba UN akosoa vikali hotuba yaTrump, aitaja kuwa ya kijahili na kijinga
Sep 20, 2017 12:51Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya lran amesema kuwa, miamala ya kijahili, michafu, chuki na iliyokosa uelewa na utoaji tuhuma zisizokuwa na msingi wowote ya Rais Donald Trump wa Marekani dhidi ya taifa la Iran katika mkutano mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA) si tu kwamba, haiendani na umoja huo, bali inakinzana pia na matakwa na matarajio ya leo ya watu wa mataifa yote ya dunia katika kikao hicho.
-
Hotuba ya kifidhuli ya Trump UN yakosolewa vikali duniani
Sep 20, 2017 03:35Matamshi ya kifedhuli aliyotoa Rais Donald Trump wa Marekani katika hotuba yake ya kwanza katika mkutano mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA) yamekosolewa vikali na viongozi na shakhsia mbalimbali wa kisiasa duniani.
-
Iran yatoa jibu kwa matamshi ya kilaghai ya Netanyahu katika UNGA
Sep 20, 2017 02:58Mshauri wa ofisi ya uwakilishi wa kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema matamshi dhidi ya Iran aliyotoa Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel katika mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ni ya kinafiki na ya kilaghai.
-
Matakwa mapya ya kufanyiwa marekebisho muundo wa Umoja wa Mataifa
Sep 19, 2017 23:21Ikiwa ni katika harakati mpya, wawakilishi wa nchi 128 wametia saini mpango wa kutaka marekebisho yafanyike katika muundo wa Umoja wa Mataifa.
-
Mkutano wa 72 wa Baraza Kuu la UN waanza leo New York
Sep 19, 2017 11:34Mkutano wa 72 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa umefunguliwa leo mjini New York nchini Marekani kwa hotuba ilioyotolewa na Katibu Mkuu wa umoja huo António Guterres.
-
UN yataka kufanyike uchunguzi kuhusu mgogoro wa Myanmar
Sep 19, 2017 11:07Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa limetaka kupewa uwezo kamili wa kuchunguza mgogoro wa sasa wa Myanmar bila ya mpaka wala kizuizi.
-
Rais Rouhani wa Iran aelekea New York katika mkutano wa UN
Sep 17, 2017 03:21Rais Hassan Rouhani wa Iran amesema makubaliano ya nyuklia yanayojulikana kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA) ni kwa maslahi ya amani na uthabiti sio tu kwa eneo hili la Mashariki ya Kati bali kwa dunia nzima.
-
UN yataka kuongezwa askari wa kulinda amani Jamhuri ya Afrika ya Kati
Sep 17, 2017 03:10Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Afrika ya Kati kimetoa mwito wa kutumwa katika nchi hiyo mamia ya askari zaidi ili kujaza pengo lililoachwa baada ya Uganda kuwaondoa wanajeshi wake nchini humo.
-
Chama tawala Burundi kimelalamikia ripoti ya UN kuhusu haki za binadamu
Sep 17, 2017 00:08Chama tawala nchini Burundi kimelalamikia ripoti ya Umoja wa Mataifa iliyoitaka Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) ifanye uchunguzi kuhusu jinai zilizofanywa na viongozi wa Burundi dhidi ya raia wa nchi hiyo.