-
Amnesty International yataka mataifa ya Ulaya yaisusie kikamilifu Israel
May 22, 2025 09:21Shirika la Msamaha Duniani la Amnesty International limetoa wito wa kususiwa kabisa utawala wa Kizayuni wakati huu ambapo baadhi ya mataifa ya bara Ulayaa yanachukua hatua za kuutenga utawala huo kutokana na jinai zake huko Gaza.
-
Umoja wa Ulaya na juhudi za kupata washirika wapya wa kibiashara
May 06, 2025 22:49Vitendo vya Rais Donald Trump wa Marekani hususan kuanza kwa vita vya kibiashara na dunia ambavyo vimesababisha machafuko katika mfumo wa uchumi na biashara wa kimataifa, vimeufanya Umoja wa Ulaya kutaka kupanua na kuimarisha uhusiano wake na nchi za Bahari ya Pasifiki (Trans-Pacific).
-
Kremlin: Umoja wa Ulaya unataka vita, sio mazungumzo
Apr 24, 2025 23:16Msemaji wa Ikulu ya Russia (Kremlin), Dmitry Peskov amesema Umoja wa Ulaya umekuwa ukizuia juhudi za kidiplomasia za Washington na Moscow kwa ajili ya kumaliza mzozo wa Ukraine, na badala yake unafanya jitihada za kurefusha uhasama na mzozo huo.
-
Mgogoro unaoshadidi wa Chuki dhidi ya Uislamu barani Ulaya
Apr 13, 2025 23:02Baada ya kuanza vita vya utawala haramu wa Israel dhidi ya Gaza, ripoti zinaonesha ongezeko la asilimia 140 ya uhalifu wa chuki dhidi ya Waislamu katika nchi za Ulaya, hasa Ujerumani — jambo ambalo limegeuka kuwa tishio kubwa kwa jamii za Ulaya.
-
Vita vya ushuru kati ya Marekani na China: Beijing kukabiliana na ubabe wa Washington
Apr 12, 2025 22:48Rais Xi Jin Ping wa China amesisitiza katika mazungumzo na Pedro Sanchez, Waziri Mku wa Uhispania ulazima wa kuimarisha ushirikiano kati ya China na Umoja wa Ulaya ili kukabiliana na hatua za upande moja za Marekani.
-
Hitilafu za viongozi wa Ulaya kuhusu jibu la vita vya ushuru vya Trump
Apr 07, 2025 23:08Tangazo la kutoza ushuru mpya la Rais wa Marekani, Donald Trump, dhidi ya nchi 180 duniani, zikiwemo nchi za Umoja wa Ulaya, limeibua hisia tofauti kutoka kwa nchi mbalimbali duniani.
-
Tehran yaihutubu EU: Shughulikieni jinai za Israel badala ya kutoa madai ya kinafiki
Mar 27, 2025 07:38Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Iran, Esmaeil Baghaei amemkosoa vikali mkuu mpya wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya, Kaja Kallas, kutokana na matamshi yake ya karibuni ya kuitaja Iran kama "tishio" wakati wa ziara yake ya karibuni katika maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu na Israel.
-
Mapatano mapya ya nchi za Umoja wa Ulaya dhidi ya Russia
Mar 24, 2025 07:04Kwa kutilia maanani jaribio la utawala wa Trump la kuanzisha usitishaji vita nchini Ukraine kwa kuilazimisha ikubali masharti yaliyowekwa na Russia na upinzani wa nchi za Umoja wa Ulaya dhidi ya suala hili, na kwa upande mwingine madai ya baadhi ya viongozi wa Ulaya kuhusu vitisho vya Russia dhidi ya bara hilo, nchi hizo sasa zimechukua hatua mpya kwa ajili ya kukabiliana na Moscow.
-
Balozi wa Trump: Russia haitaki kushambulia Ulaya
Mar 22, 2025 23:10Mjumbe maalum wa Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati (Asia Magharibi), Steve Witkoff amepuuzilia mbali madai kwamba Russia ina nia ya kuzivamia nchi nyingine za Ulaya, akisisitiza kuwa hofu hizo ni za "kipuuzi".
-
Wanachama wa EU wakubaliana kuongeza nguvu za kijeshi mkabala wa Russia
Mar 22, 2025 01:03Waziri Mkuu wa Poland amesema kuwa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa zimekubaliana hadi kufikia mwaka 2030 kuongeza uwezo wao wa kijeshi ili kuweza kukabiliana na mshambulizi yoyote ya Russia.