-
Mashtaka dhidi ya utawala wa Biden katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu
Feb 26, 2025 23:06Taasisi ya "Demokrasia kwa ajili ya Ulimwengu wa Kiarabu Sasa" (DAWN), imefungua mashtaka dhidi ya Rais wa zamani wa Marekani, Joe Biden na mawaziri wake wawili yaani waziri wa zamani wa mambo ya nje wa Marekani, Anthony Blinken na waziri wa zamani wa ulinzi wa nchi hiyo Lloyd Austin katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu, ikiitaka ianzishe uchunguzi dhidi ya viongozi hao kutokana na kusaidia uhalifu wa kivita wa utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
HAMAS: Mwafaka umefikiwa kuhusu Wapalestina 620 ambao Israel ilichelewesha kuwaachia huru
Feb 26, 2025 09:28Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imesema, ujumbe wake umehitimisha ziara yake katika mji mkuu wa Misri Cairo na umefikia makubaliano na wapatanishi ya kutatuliwa ucheleweshaji uliofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel wa kuwaachilia huru wafungwa Wapalestina ambao ilipasa waachiliwe siku ya Jumamosi iliyopita kama sehemu ya makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya pande hizo mbili.
-
Misri yakataa pendekezo la Wazayuni la kuitawala Gaza kwa miaka 8
Feb 26, 2025 03:10Cairo imekataa pendekezo la maafisa wa utawala za Kizayuni wa Isarel wanaotaka serikali ya Misri isimamia mamlaka ya Ukanda wa Gaza kwa miaka 8 hadi 15.
-
Watoto wachanga watano wafariki Ghaza kutokana na mgando wa baridi kali
Feb 25, 2025 07:29Watoto wachanga watano wamefariki dunia katika Ukanda wa Ghaza kutokana na mgando wa baridi kali katika eneo hilo lililowekewa mzingiro na utawala wa Kizayuni wa Israel na kuzuiwa kuingizwa misaada ya kibinadamu ikiwemo ya vifaa vya huduma za tiba.
-
Kuendelea mashambulizi na jinai za Wazayuni kaskazini mwa Ukingo wa Magharibi
Feb 24, 2025 22:58wanajeshi wa utawala wa Kizayuni kwa mara nyingine tena wameshambulia maeneo mbalimbali katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Afrika Kusini: Usitishaji vita Gaza sharti ulete amani ya kudumu
Feb 20, 2025 23:20Rais wa Afrika Kusini amesema usitishaji wa mapigano katika Ukanda wa Gaza unapasa kuleta uadilifu na amani ya kudumu katika eneo hilo.
-
Matakwa ya mashirika ya haki za binadamu ya kutopatiwa Israel vipuri vya ndege za kivita za F-35
Feb 20, 2025 22:53Muungano wa Kimataifa wa mashirika 232 ya kutetea haki za binadamu umezitaka nchi mbalimbali zinazohusika katika uundaji za ndege za kivita aina ya F-35 kuacha kuipatia Israel vipuri vya ndege hizo.
-
Errea nayo yabatilisha mkataba wake na Shirikisho la Soka la utawala wa Kizayuni
Feb 20, 2025 04:08Kampuni nyingine ya udhamini wa vifaa vya michezo ya Ulaya imefuta mkataba wake na Shirikisho la Soka la utawala wa Kizayuni wa Israel na hivyo kutoa pigo jingine kwa utawala huo haramu.
-
Kuendelea kushtakiwa jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina
Feb 19, 2025 23:04Gideon Sa’ar Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa utawala vamizi wa Israel ameshtakiwa kwa kutenda jinai za kivita katika Ukanda wa Gaza.
-
Ripoti: Marekani na Ufaransa zinataka askari mamluki wapelekwe kusini mwa Lebanon
Feb 19, 2025 03:24Marekani na Ufaransa zimeripotiwa kuwa zimependekeza mamluki wanaoitwa wakandarasi binafsi wapelekwe kusini mwa Lebanon katika jitihada za kuushawishi utawala wa Kizayuni wa Israel uondoe kikamilifu majeshi yake nchini humo.