-
NAM yaonya kuhusu chokochoko za Washington; Je, Marekani iko mbioni kushambulia Venezuela?
Oct 19, 2025 02:40Wakati ripoti zikionyesha kuwa Pentagon inatayarisha machaguo ya kijeshi dhidi ya Venezuela, Jumuiya ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote (NAM), ambayo inaundwa na zaidi ya nchi 120, imeonya kwamba shambulio lolote dhidi ya nchi hiyo ya Amerika Kusini litakuwa ukiukaji wa wazi wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa.
-
Venezuela yatangaza 'maeneo mapya ya ulinzi' mpaka wa Colombia
Oct 16, 2025 09:41Rais wa Venezuela, Nicolás Maduro amesisitiza kujitolea kwa taifa lake kwa amani, uhuru na utu, akizindua mpango mpya wa kuimarisha ulinzi wa ardhi ya nchi hiyo, huku Marekani ikiidhinisha operesheni za CIA katika eneo hilo.
-
Balozi: US inaihangaisha dunia kwa kisingizio cha kuleta 'uhuru'
Oct 15, 2025 02:32Balozi wa Venezuela nchini Iran, José Rafael Silva Aponte amesema Marekani inaihangaisha dunia nzima, ikiwa ni pamoja na Amerika ya Kusini, kwa kutumia kisingizio cha kuleta uhuru katika maeneo tofauti ya dunia, lakini Venezuela daima itasalia kuwa nchi huru na yenye mamlaka ya kujitawala.
-
Amerika ya Kusini yagawanyika juu ya kiongozi wa upinzani Venezuela kutunukiwa Tuzo ya Amani ya Nobel
Oct 12, 2025 05:24Kutunukiwa Tuzo ya Amani ya Nobel kiongozi wa upinzani nchini Venezuela María Corina Machado kumeibua hisia tofauti katika nchi za Amerika Kusini, huku baadhi ya viongozi wa nchi za eneo hilo wakipongeza hatua hiyo na wengine kulaani vikali kwa kuashiria matamshi na vitendo vya Machado vya kuchochea vurugu na machafuko au hata kuunga mkono kufanywa mashambulio na uvamizi wa kigeni dhidi ya nchi yake mwenyewe.
-
Venezuela: Netanyahu mtenda jinai anaendelea kuhujumu jitihada za amani
Oct 05, 2025 10:49Yván Gil Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela amemtaja Benjamin Netanyahu Waziri Mkuu wa Israel kama muuaji sugu anayeendelea kuhujumu jitihada za kuhitimisha vita huko Gaza.
-
Venezuela kutangaza 'hali ya hatari' iwapo itavamiwa na Marekani
Oct 01, 2025 02:32Serikali ya Venezuela imetangaza kuwa itaamilisha "Dikrii ya Dharura ya Kigeni" ikiwa Marekani itaanzisha mashambulizi yoyote ya kijeshi dhidi ya nchi hiyo.
-
Waziri wa Ulinzi wa Venezuela aonya askari wa US: Msiwe wapumbavu
Sep 15, 2025 11:20Waziri wa Ulinzi wa Venezuela, Vladimir Padrino López amelaani kitendo cha Marekani cha kupeleka vikosi vyake vya majini kwenye visiwa vya Caribbean kwa kisingizio kupambana na ulanguzi wa dawa za kulevya, akisisitiza kuwa lengo halisi la Washington ni kuangusha serikali halali ya Rais Nicolas Maduro.
-
Maduro aonya: Tutaingia kwenye ‘mapambano ya silaha’ ikiwa tutashambuliwa na US
Sep 06, 2025 11:38Rais wa Venezuela, Nicolas Maduro ameonya kwamba nchi yake itagura kutoka kwenye siasa na kuingia kwenye "mapambano ya kutumia silaha" iwapo Marekani itaanzisha mashambulizi ya kijeshi dhidi ya taifa hilo.
-
Maduro: Tutaitangaza Venezuela 'jamhuri yenye silaha' ikiwa US itatushambulia
Sep 02, 2025 07:03Rais wa Venezuela, Nicolas Maduro amesema kuongezeka uwepo wa majeshi ya Marekani katika eneo la Caribbean kunalenga kuipindua serikali yake, na kusisitiza kuwa yuko tayari "kutangaza jamhuri yenye silaha" ikiwa nchi hiyo itashambuliwa na wanajeshi hao wavamizi.
-
Kwa nini Rais wa Colombia ametahadharisha kuhusu njama za Marekani za kuigeuza Venezuela kuwa Syria nyingine?
Aug 23, 2025 03:58Rais wa Colombia ametahadharisha kuwa Marekani inaweza kuifanya Venezuela kuwa Syria nyingine.