Apr 15, 2018 13:28
Katika kikao cha viongozi wa nchi za Amerika kilichofanyika mjini Lima nchini Peru, Michael Pence sambamba na kuashiria kwamba Marekani haitoendelea kufumbia macho matukio yanayojiri nchini Venezuela, amesisitiza juu ya kuendelezwa mashinikizo dhidi ya serikali ya nchi hiyo.