-
Venezuela yamtimua balozi wa Ujerumani kwa hatua yake ya kumuunga mkono Juan Guaidó
Mar 07, 2019 00:38Wizara ya Mambo ya Nje ya Venezuela imemtimua balozi wa Ujerumani nchini humo kutokana na hatua yake ya kumuunga mkono Juan Guaidó, mpinzani wa serikali aliyejitangaza kuwa rais, badala ya serikali halali ya Caracas.
-
Lavrov: Matamshi ya Bolton dhidi ya Venezuela ni ya udhalilishaji
Mar 04, 2019 23:13Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia ameyataja matamshi yaliyotolewa na Mshauri wa Usalama wa Taifa wa Marekani dhidi ya Venezuela kuwa ni udhalilishaji kwa Amerika ya Latini.
-
Kiongozi wa upinzani Venezuela anakabiliwa na kifungo cha miaka 30 jela
Feb 27, 2019 04:34Juan Guaidó, kiongozi wa upinzani aliyejitangaza kuwa rais wa mpito wa Venezuela anaandamwa na kifungo cha miaka 30 jela.
-
Rais Maduro: Marekani sasa inafanya njama za kuanzisha vita Venezuela
Feb 27, 2019 01:15Rais Nicolás Maduro wa Venezuela amesema kuwa hivi sasa serikali ya Marekani inafanya njama za kuwasha moto wa vita katika eneo la Amerika ya Latini hususan nchini Venezuela.
-
Tishio la kijeshi; kuendelea hatua zilizogonga mwamba za Marekani dhidi ya Venezuela
Feb 26, 2019 23:13Sambamba na kuongezeka harakati za kijeshi za Marekani dhidi ya Venezuela, Rais Nicolas Maduro wa nchi hiyo ameituhumu Washington kwamba, inafanya njama za kuzusha mgogoro kwa shabaha ya kuanzisha vita katika eneo la Amerika ya Latini.
-
Amir-Abdollahian: Marekani inataka kuzusha machafuko nchini Venezuela
Feb 25, 2019 23:07Msaidizi maalumu wa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika masuala ya kimataifa amelaani hatua ya Marekani ya kuingilia masuala ya ndani ya Venezuela na kusema kuwa, Washington inataka kuiondoa madarakani serikali halali na kuitumbukiza nchi hiyo katika vurugu na machafuko.
-
Marekani yadai siku za Maduro kuwa madarakani Venezuela zinahesabika
Feb 25, 2019 00:50Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani ameonya kuwa, Washington itaendelea kuisakama na kuishinikiza serikali ya Venezuela hadi ifahamu kuwa siku zake za kutawala zinahesabika.
-
Iran kutuma misaada Venezuela
Feb 25, 2019 00:50Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iko tayari kutuma msaada wa dawa na vifaa vya kitiba Venezuela, nchi ambayo imekuwa ikikabiliwa na njama za mababeru wakiongozwa na Marekani ambao wanataka kuipindua serikali ya Rais Nicolas Maduro.
-
Maduro: Wananchi wa Venezuela watasimama imara kupambana na madola ya kibeberu
Feb 23, 2019 13:01Rais Nicolas Maduro wa Venezuela amesema kuwa serikali ya Caracas kwa ushirikiano na wananchi wa nchi hiyo watasimama kidete kupambana na madola ya kibeberu na hawatorudi nyuma katika suala hilo.
-
Venezuela yatoa mwito wa kuungwa mkono na UN kukabiliana na "Hujuma ya Kijeshi"
Feb 21, 2019 21:39Ofisi ya uwakilishi ya Venezuela katika Umoja wa Mataifa imewaalika mabalozi wa nchi 46 wanacjama kushiriki kikao ambacho lengo lake ni kuutaka umoja huo utimize wajibu wake wa kupinga vitisho vya uanzishaji "hujuma ya kijeshi".