Jul 11, 2021 08:22
Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron ameonana na wakuu wa nchi tano za eneo la Sahel ya Afrika ambazo ni Chad, Mali, Burkina Faso, Mauritania na Niger. Ingawa kikao hicho kimefanyika kwa njia ya Intaneti, lakini Rais Mohammad Bazoum wa Niger yeye ameshiriki kikao hicho akiwa ziarani nchini Ufaransa.