-
Iran yatahadharisha kuhusu Marekani kulitumia vibaya Baraza la Usalama la UN
May 20, 2026 11:06Mwakilishi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa ameeleza kuwa: "Marekani inalitumia vibaya Baraza la Usalama kwa kueneza uwongo na tuhuma zisizo na msingi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na mpango wake wa nyuklia."
-
'Hatutasalimu amri kamwe': Pezeshkian aapa kuendeleza mapambano huku Trump akizidi kupiga ngoma za vita
May 19, 2026 05:51Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, ameapa kutosalimu amri kamwe mbele ya dola lolote au kutoa kafara heshima ya taifa kwa ajili ya faraja.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran awaonya maadui, mkijaribu mtashindwa tena
May 15, 2026 09:48Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi, amezionya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel kuhusu kuanzisha tena hatua mpya za kijeshi dhidi ya Iran, akisema kuwa makabiliano ya awali yalishindwa kufikia malengo yaliyokusudiwa, na kwamba jaribio lolote la baadaye litakuwa na matokeo yaleyale.
-
Nchi Washirika wa Marekani katika Ghuba ya Uajemi wagawanyika kuhusu vita vipya dhidi ya Iran
May 15, 2026 04:48Tathmini ya siri iliyofanywa na shirika la kijasusi la Marekani, CIA, imebaini kuwa washirika wa Marekani katika eneo la Ghuba ya Uajemi wamegawanyika kuhusu iwapo waunge mkono vita vipya dhidi ya Iran.
-
Washington Katika Mkwamo
May 15, 2026 07:40Jarida la Marekani la The Atlantic hivi karibuni lilichapisha ripoti iliyochunguza kwa mapana na marefu vipengele vya makabiliano ya kijeshi kati ya Marekani na Iran pamoja na athari zake. Ripoti hiyo inaonyesha kuwa, sera na hatua za Washington hadi sasa hazijawa na matokeo yaliyotarajiwa, na zimeisababishia Marekani vizuizi na changamoto kali.
-
Spika Qalibaf: Majeshi ya Iran yako tayari kuwashitua wavamizi
May 12, 2026 09:13Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Qalibaf, amesema kuwa majeshi ya Jamhuri ya Kiislamu yako katika hali ya juu kabisa ya utayari wa kivita na yako tayari kutoa jibu kali, la haki na linalostahili dhidi ya aina yoyote ya uchokozi. Amewaonya maadui kwamba mikakati na maamuzi yenye makosa hayatazaa chochote isipokuwa maafa.
-
Kurudi Nyumbani Wakati wa Vita vya Siku 40 Wairan Waliokuwa Wameihajiri Nchi Kunafikisha Ujumbe Gani?
May 09, 2026 14:04Takwimu zilizorekodiwa katika mipaka ya Iran zinaonyesha kuwa wakati wa vita vya siku 40 vilivyoanzishwa na Marekani na utawala wa Kizayuni dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Wairani 630,000 waliingia nchini kupitia mipaka ya nchi kavu.
-
Pezeshkian amwambia Macron: Iran yataka diplomasia huku ikisisitiza kulinda haki za taifa
May 07, 2026 08:07Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, amemwambia mwenzake wa Ufaransa, Emmanuel Macron, kuwa Tehran iko tayari kuendelea kwa dhati na njia za kidiplomasia ili kukomesha vita, huku ikisisitiza umuhimu wa kulindwa haki za taifa la Iran.
-
Papa Leo aendelea kuponda bwabwaja za Trump
May 06, 2026 10:52Mvutano kati ya Rais Donald Trump wa Marekani na Kiongozi wa Wakatoliki duniani Papa Leo wa XIV kuhusu misimamo ya kupinga vita unaendelea kutokota.
-
Manowari kubwa na ya kisasa zaidi ya Marekani yaondoka kwa fedheha katika vita dhidi ya Iran
May 02, 2026 11:31USS Gerald R. Ford, meli kubwa zaidi ya kivita na ya gharama ya juu kuwahi kuundwa na Marekani, imelazimika kujiondoa kutoka ukanda wa Asia Magharibi baada ya siku 309 za operesheni endelevu baharini, ikiwa katika jukumu la kuunga mkono vita dhidi ya Iran.