May 16, 2016 06:54
Donald Trump, mgombea wa kiti cha urais wa chama cha Republican nchini Marekani kwa mara nyingine tena ametoa matamshi yanayodhihirisha misimamo yake ya chuki na ya kibaguzi dhidi ya Uislamu na wageni. Trump amedai kuwa wakimbizi wa Syria nchini Marekani wanapanga njama ya kufanya shambulizi la kigaidi kama la Septemba 11.