Vyombo vya habari vya Kenya vimefichua kuwa, mabadiliko ya siri yaliyotayarishiwa miswada ya kufanikisha utekelezaji wa ripoti ya Kamati ya Kitaifa ya Mazungumzo (NADCO) iliyowasilishwa majuzi katika Seneti ya nchi hiyo yamefuchua njama ya kuvunja chama cha Azimio la Umoja-One Kenya kinachoongozwa na Raila Odinga.
Chama cha Succès cha Masra Waziri Mkuu wa Chad ambaye ni mmoja wa wagombea wa urais aliyechuana katika uchaguzi Jumatatu wiki hii jana kililaani ghasia na vitisho dhidi yake na wafuasi wake, na kudai kuwa uchaguzi wa rais uligubikwa na udanganyifu.
Marekani ndiyo muungaji mkono mkubwa zaidi wa utawala wa Kizayuni wa Israel ambapo serikali ya Biden imetoa msaada mkubwa zaidi wa kijeshi na silaha kwa Tel Aviv wakati wa vita vya Gaza, ambavyo vimeingia katika mwezi wake wa saba.
Kwa mara nyingine tena, mwanasiasa wa upinzani nchini Uganda ambaye pia alikuwa mgombea urais wa chama cha upinzani cha NUP katika uchaguzi uliopita, Robert Kyagulanyi, maarufu kama Bobi Wine, amekamatwa mjini Entebbe.
Watu kadhaa wameuawa huku wengine wengi wakijeruhiwa nchini Senegal, katika maandamano ya ghasia ya wafuasi wa kiongozi wa upinzani nchini humo Ousmane Sonko, ambaye karibuni alihukumiwa kifungo cha miaka miwili jela.
Kufuatia maandamano ya maelfu ya watu wanaoipinga familia ya kifalme ya Uingereza katika mji wa London, mbunge mmoja wa ngazi ya juu wa chama tawala cha kihafidhina cha nchi hiyo, ametoa matamshi yenye utata, akitaka wapinzani hao wafukuzwe nchini ikiwa hawawezi kumkubali mfalme wa nchi hiyo.
Kiongozi wa upinzani nchini Tanzania Tundu Lissu amerejea nyumbani kutoka uhamishoni baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuondoa marufuku ya mikutano ya kisiasa ya hadhara.
Nchi za Magharibi, kinyume na nara na kaulimbiu zao za kizandiki za kutetea utu na ahadi zao za kusimamia kidemokrasia, zimeshakiuka mara nyingi misingi hiyo; na sio tu haziwezi kuwavumilia wapinzani na wakosoaji wao, bali hutumia pia njia mbalimbali kuzima sauti zao au hata kuwamaliza moja kwa moja.
Serikali ya Ufaransa Jumanne wiki hii ilidokeza uwezekano wa kutazamwa umpya mpango tata wa Rais Emmanuel Macron wa kubadilisha sheria za pensheni. Hatua hiyo inaonekana kuwa ni kusalimu amri mbele ya wapinzani wa mpango huo.
Mgogoro wa kisiasa nchini Tunisia umechukua sura na muelekeo mpana zaidi baada ya kuvunjika mazungumzo baina ya serikali na muungano wa asasi za ajira, ambao ndio mwamvuli mkubwa zaidi wa miungano mbalimbali inayopinga sera za serikali ya sasa ya nchi hiyo; na sasa muungano huo umewatolea mwito wananchi kushiriki kwenye mgomo wa umma wa nchi nzima.