-
Afrika Kusini kugeukia Russia, Iran kwenye mradi wake wa nyuklia?
Feb 18, 2025 04:02Afrika Kusini imesema huenda itashirikiana na Russia au Iran katika juhudi za kupanua uwezo wake wa nishati ya nyuklia.
-
Pezeshkian: Silaha za nyuklia hazina nafasi katika doktrini ya Jamhuri ya Kiislamu
Feb 06, 2025 23:24Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian amesema nchi yake haifuatilii vita wala silaha za nyuklia, kwani mafundisho ya Jamhuri ya Kiislamu yanakataa mauaji ya watu wasio na hatia kwa hali yoyote.
-
Muhusika wa faili la nyuklia la Iran: Tehran inatetea kwa nguvu zote mpango wake wa amani wa nyuklia
Feb 04, 2025 05:04Mshauri wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu na muhusika wa faili la nyuklia la Iran amesema: Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inatetea kwa nguzu zote mpango wake wa nyuklia unaotekelezwa kwa malengo ya kiraia.
-
CIA yakiri kwamba mradi wa nyuklia wa Iran ni wa amani
Jan 11, 2025 23:33Mkuu wa shirika la kijasusi la Marekani (CIA) amekiri kwamba mradi wa nyuklia wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni wa kiraia na hakuna ushahidi wowote unaoonesha kuwa mradi huo umeelekea upande wa kijeshi.
-
Muhammad Islami: Wazayuni wameulemaza Umoja wa Mataifa
Dec 17, 2024 23:28Mkuu wa Taasisi ya Nishati ya Atomiki ya Iran amesema kuwa, kivitendo Wazayuni wameulemaza Umoja wa Mataifa na taasisi hiyo iliyokuwa ikipigania haki za binadamu na uadilifu hivi sasa imepoteza kabisa ufanisi na uutendaji wake.
-
Iran yaipongeza IAEA kwa kukiri kuwa Israel ina silaha za nyuklia, yataka ilazimishwe kuharibu silaha hizo
Dec 13, 2024 00:11Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayehusika na Masuala ya Kimataifa na Kisheria amejibu hatua ya kukiri Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki kuhusu hatari za silaha za nyuklia za utawala wa Kizayuni, na kuutaka wakala huo ushughulikie silaha za nyuklia za Israel na sio kuusakama mradi wa matumizi ya amani wa nyuklia wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Iran: Mpango wa amani wa nyuklia wa Iran uko uwazi na chini ya usimamizi wa IAEA
Dec 08, 2024 04:33Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amesema kuwa, mradi wa amani wa nyuklia wa Iran uko wazi na unafanyika chini ya usimamizi wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA).
-
Iran yapinga madai ya 'Troika ya Ulaya' kuhusu kadhia ya nyuklia
Dec 04, 2024 23:27Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amemtumia barua Katibu Mkuu wa umoja huo na Baraza la Usalama akisema kuwa tuhuma zilizotolewa dhidi ya Tehran hazina msingi wowote na zina malengo ya kisiasa. Amir Saeid Iravani ameeleza hayo kufuatia tuhuma zilizotolewa na wawakilishi wa Troika ya Ulaya dhidi ya Tehran. Troika hiyo inajumuisha Ufaransa, Uingereza na Ujerumani.
-
Tuhuma na misimamo ya kurudiwarudiwa ya Marekani kwa ulimi wa Joe Biden katika Umoja wa Mataifa
Sep 26, 2024 00:28Jumanne ya wiki hii, rais wa Marekani, Joe Biden, alitoa hotuba yake ya mwisho katika kikao cha 79 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York na kukariri madai ya uongo ya siku zote dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na dhidi ya kambi ya Muqawama. Rais wa Marekani alidai kuwa eti serikali yake inapigania kuleta amani na utulivu katika ukanda wa Asia Magharibi.
-
Balozi wa Iran UN: Maghala ya nyuklia ya Israel ni tishio kubwa kwa amani na usalama wa dunia
Sep 05, 2024 07:13Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesema, silaha za nyuklia za utawala wa Kizayuni wa Israel ni tishio kubwa kwa amani na usalama wa kikanda na wa ulimwengu mzima.