-
Zarif: Uhai wa JCPOA unategemea kufungumana kikamilifu US
Jan 11, 2018 04:24Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Tehran haitaendelea kufungamana na makubaliano ya nyuklia ya JCPOA, iwapo Marekani itayakiuka.
-
Zarif: Trump anadunisha demokrasia kwa kutishia wapinzani wake
Dec 21, 2017 00:12Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran amekosoa vikali msimamo wa Marekani wa kupinga maamuzi ya Umoja wa Mataifa kuhusu Quds tukufu na kusema kuwa: Washington imebakia katika kiwango cha "ama uwe pamoja na sisi au dhidi yetu."
-
Zarif: Iran itaishtaki Marekani Umoja wa Mataifa
Dec 17, 2017 00:16Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesisitiza kwamba Jamhuri ya Kiislamu itayawasilisha Umoja wa Mataifa madai ya Nikki Haley, balozi wa Marekani katika umoja huo kwamba eti Iran imeipatia silaha harakati ya Ansarullah ya Yemen.
-
Zarif: Uhai na kifo cha baadhi ya nchi zinazopakana Iran unategemea amri ya madola makubwa
Dec 16, 2017 12:22Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Mohammad Javad Zarif amesema uhai na kifo cha baadhi ya tawala zinazopakana na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran unategemea maamuzi ya madola makubwa au Shirika la Kijeshi ya Nchi za Magharibi (NATO), au madola makubwa ya nyuklia.
-
Zarif: Marekani ni mshirika wa Saudia katika uhalifu wa kivita Yemen
Dec 16, 2017 00:15Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran amesema kuwa Marekani ni mshirika wa Saudi Arabia katika uhalifu na jinai za kivita zinazofanyika nchini Yemen.
-
Zarif: Ni maskhara kuona Saudi Arabia ikiituhumu Iran kuwa inasababisha machafuko
Nov 19, 2017 23:19Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa ni maskhara kwa Saudia Arabia kuituhumu Iran kuwa inasababisha machafuko katika hali ambayo nchi hiyo ndiyo inayowachochea magaidi na iliyoanzisha vita huko Yemen.
-
Zarif: Iran, Russia na Uturuki zimeazimia kulinda amani endelevu huko Syria
Nov 19, 2017 12:48Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa Iran, Uturuki na Russia zikiwa ni nchi zinazosimamia mazungumzo ya Astana kwa ajili ya amani nchini Syria ziko tayari kuandaa mazingira ya kudumisha amani na usalama endelevu.
-
Zarif: Saudia inachukua hatua za kijinga na kihasama
Nov 17, 2017 23:33Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Wasaudia wanapuuza uhakika na hali halisi ya kihistoria na kuchukua hatua za kihasama na kijinga ambazo zinaendelea kuwasababishia madhara wao wenyewe.
-
Zarif amwandikia barua Katibu Mkuu wa UN; Hali ya Yemen ni mbaya sana
Nov 14, 2017 03:59Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran jana usiku alimuandikia barua Antonio Guterres Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akisema kuwa hali ya mambo nchini Yemen ni mbaya sana na inatia wasiwasi mkubwa; hiyo ikiwa ni natija ya uvamizi wa kijeshi na kuzingirwa pande zote nchi hiyo na utawala wa kidikteta wa Saudi Arabia.
-
Iran yaishukuru Jamii ya Kimataifa; Zarif: Iran ina uwezo wa kusimamia maafa ya zilzala
Nov 14, 2017 03:16Muhammad Javad Zarif, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran leo asubuhi ametoa shukrani kufuatia salamu za pole zilizotolewa kutoka maeneo mbalimbali baada ya kujiri tetemeko la ardhi magharibi mwa Iran na kufuatia pendekezo la nchi mbalimbali za kutaka kuwasaidia waathirika wa zilzala hiyo na akasema kuwa: Iran hivi sasa ina uwezo wa kushughulikia mgogoro huo wa tetemeko la ardhi kwa kustafidi na suhula za ndani.