-
Rais wa Zimbabwe awasamehe wafungwa 3,000
Mar 22, 2018 11:06Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe ambaye alichukua madaraka baada ya mtangulizi wake Robert Mugabe kulazimishwa kujiuzulu mwezi Novemba mwaka jana, amewasamehe wafungwa zaidi ya 3,000 kwa lengo la kupunguza msongamano mkubwa kwenye magereza ya nchi hiyo.
-
Mnangagwa: Fedha za Wazimbabwe zilizokuwa zimefichwa nje ya nchi zimerejeshwa
Mar 19, 2018 12:01Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe amesema leo kuwa chini ya nusu ya fedha zilizofichwa nje ya nchi na shakhsia na makampuni mbalimbali zimerejeshwa nchini baada ya kufikia ukomo muhula wa siku 90 zilizotolewa na ameonya kuwa wale wote ambao hawajawajibika watashtakiwa.
-
UN yaunga mkono kufanyika uchaguzi Julai nchini Zimbabwe
Mar 18, 2018 13:10Umoja wa Mataifa umesema kuwa unaunga mkono mpango wa kufanyika uchaguzi wa rais nchini Zimbabwe mwezi Julai mwaka huu.
-
Rais Mnangagwa amjibu Mugabe; asema Zimbabwe imesonga mbele baada ya utawala wake
Mar 17, 2018 04:16Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe amesema kuwa, nchi hiyo imeshapiga hatua baada ya kumwondoa madarakani kiongozi wa zamani wa nchi hiyo Robert Mugabe.
-
Mugabe: Sikudhani kuwa Mnangagwa atanigeuka
Mar 16, 2018 01:13Rais wa zamani wa Zimbabwe amesema kuwa hakufikiria kuwa rais wa sasa wa nchi hiyo, Emmerson Mnangagwa angemgeuka na kusimama dhidi yake na amelaani hatua ya Mnangagwa ya kumuondoa madarakani kwa njia ya mapinduzi.
-
Wasiwasi watanda Zimbabwe baada ya Mugabe kuonekana kuunga mkono mpinzani
Mar 09, 2018 03:42Wasiwasi umetanda katika chama tawala nchini Zimbabwe, ZANU-PF, baada ya rais wa zamani Robert Mugabe kuonekana hadharani akiwa ameandamana na jenerali mstaafu ambaye yuko katika kambi ya upizani na ambaye anapanga kuwania urais baadaye mwaka huu.
-
Mfuasi wa Mugabe aunda chama kipya cha siasa Zimbabwe kuchuana na rais Mnangagwa katika uchaguzi
Mar 05, 2018 22:58Ambrose Mutinhiri, jenerali mstaafu wa jeshi la Zimbabwe na mfuasi wa aliyekuwa rais wa nchi hiyo Robert Mugabe ameunda chama kipya cha siasa kinachojulikana kama Harakati Mpya ya Kizalendo (NFP) kuchuana na rais Emmerson Mnangagwa katika uchaguzi mkuu ujao.
-
Maelfu ya Wazimbabwe wauaga mwili wa 'Jenerali wa Watu' Tsvangirai; maziko yake kufanyika leo
Feb 20, 2018 04:49Shughuli ya kutoa heshima na kuuaga mwili wa aliyekuwa kiongozi wa chama kikuu cha upinzani nchini Zimbabwe MDC Morgan Tsvangirai imefanyika kwenye viunga vya mji mkuu Harare.
-
Uingereza kuwatimua maelfu ya wahajiri wa Zimbabwe
Feb 16, 2018 23:10Serikali ya Uingereza imetangaza azma yake ya kuwafukuza nchini humo maelfu ya wahajiri haramu raia wa Zimbabwe.
-
Rais wa Zimbabwe amteua Jaji wa Mahakama Kuu kuwa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi
Jan 31, 2018 23:09Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe amemteua Jaji wa Mahakama Kuu Priscilla Chigumba kuwa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi wakati nchi hiyo inajiandaa kwa uchaguzi mkuu muhimu ambao itibari yake inatazamiwa kuwa na umuhimu mkubwa katika kujenga tena uhusiano wake wa nje.