-
Uingereza kuwatimua maelfu ya wahajiri wa Zimbabwe
Feb 16, 2018 23:10Serikali ya Uingereza imetangaza azma yake ya kuwafukuza nchini humo maelfu ya wahajiri haramu raia wa Zimbabwe.
-
Rais wa Zimbabwe amteua Jaji wa Mahakama Kuu kuwa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi
Jan 31, 2018 23:09Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe amemteua Jaji wa Mahakama Kuu Priscilla Chigumba kuwa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi wakati nchi hiyo inajiandaa kwa uchaguzi mkuu muhimu ambao itibari yake inatazamiwa kuwa na umuhimu mkubwa katika kujenga tena uhusiano wake wa nje.
-
Rais wa Zimbabwe: Nitaheshimu matokeo ya uchaguzi wa rais
Jan 24, 2018 11:09Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe ameahidi kuwa nchi hiyo itafanya uchaguzi wa urais kabla ya Julai mwaka huu na kwamba ataheshimu uamuzi wa wananchi.
-
Chama tawala Zimbabwe chawatimua bungeni wafuasi 11 wa Mugabe
Jan 19, 2018 04:17Chama tawala nchini Zimbabwe ZANU-PF kimewafukuza bungeni waitifaki na wafuasi 11 wa aliyekuwa rais wa nchi hiyo Robert Mugabe, huku rais mpya Emmerson Mnangagwa akiendelea kuwatimua maafisa waliomuunga mkono hadharani Mugabe na mkewe Grace.
-
Rais Mnangagwa: Uchaguzi wa Zimbabwe kufanyika baada ya miezi minne au mitano
Jan 19, 2018 00:57Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe ametangaza kuwa, uchaguzi mkuu wa nchi hiyo utafanyika katika kipindi cha miezi minne au mitano ijayo.
-
Mawaziri wawili wa serikali iliyopita ya Zimabwe wafunguliwa mashtaka ya ufisadi
Jan 06, 2018 13:26Mawaziri wawili waliohudumu katika serikali ya aliyekuwa rais wa Zimbabwe Robert Mugabe wamefunguliwa mashtaka ya ufisadi, katika kile kinachoonekana kama hatua ya kuwakandamiza maafisa waaminifu kwa Mugabe.
-
Rais wa Zimbabwe abadilisha msimamo kuhusu serikali ya umoja wa kitaifa
Jan 05, 2018 23:30Habari kutoka nchini Zimbabwe zinasema kuwa rais wa nchi hiyo amekubaliana na mpango wa kuweko serikali ya umoja wa kitaifa nchini humo.
-
Maveterani Zimbabwe: Jeshi kama lingechelewa kumtimua Mugabe, tungemtimua sisi
Dec 29, 2017 12:33Mashujaa wa vita vya ukombozi nchini Zimbabwe wametangaza kwamba, walikuwa wamepanga mkakati wa kumuondoa madarakani rais wa zamani wa nchi hiyo, Robert Mugabe wiki chache kabla ya jeshi kumtimua.
-
Mkuu wa zamani wa vikosi vya ulinzi Zimbabwe aapishwa; Mugabe nae apatiwa haki za kidiplomasia
Dec 29, 2017 00:11Mkuu wa vikosi vya ulinzi wa Zimbabwe aliyejiuzulu ambaye aliongoza mapinduzi yasiyo ya umwagaji damu na kuhitimisha utawala wa miaka 37 wa Robert Mugabe jana Alhamisi aliapishwa kuwa Makamu wa Rais wa nchi hiyo na hivyo kuwa kiongozi wa ngazi ya juu zaidi wa kijeshi kuingia serikalini.
-
Mkuu wa majeshi ya Zimbabwe aliyejiuzulu kuapishwa kuwa makamu wa rais
Dec 28, 2017 04:28Aliyekuwa Kamanda wa Vikosi vya Ulinzi nchini Zimbabwe Jenerali Constantino Chiwenga ambaye aliongoza mapinduzi baridi ya kijeshi dhidi ya Robert Mugabe anatazamiwa kuapishwa leo Alkhamisi kuwa makamu wa Rais Emmerson Mnangagwa wa nchi hiyo.