Ould Sheikh apinga serikali ya Uokovu wa Kitaifa Yemen
Mjumbe wa Umoja wa Mataifa katika Masuala ya Yemen amedai kuwa hatua ya Harakati ya Ansarullah ya kuunda serikali mpya ya Uokovu wa Kitaifa nchini humo haiisaidii chochote nchi hiyo wala kusogeza mbele mchakato wa amani nchini humo.
Ismail Ould Sheikh Ahmad amedai kuwa hatua hiyo ya Harakati ya Ansarullah inatoa pigo kwa juhudi zilizofanyika hadi sasa kwa uungaji wa Umoja wa Mataifa kwa lengo la kuhitimisha mgogoro na vita vya miezi 20 huko Yemen. Mjumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Yemen pia amedai kuwa kundi la Ansarullah na chama cha Congresi ya Wananchi ya Yemen haviko kwa maslahi ya Wayemeni hivi sasa bali makundi hayo yanaifanya hali ya mambo nchini humo kuwa mbaya zaidi. Harakati ya Ansarullah na Congresi ya wananchi ya Yemen yenye mfungamano na Ali Abdallah Saleh juzi ziliasisi Serikali ya Uokovu wa Kitaifa ya nchi hiyo kwa kuhudhuriwa na mawaziri 42 chini ya uenyekiti wa Abdulaziz bin Habtoor Mkuu wa serikali hiyo mpya.

Mkuu wa Baraza Kuu la Mapinduzi Yemen amesema baraza la mawaziri litajumuisha majina yaliyowasilishwa na Harakati ya Ansarullah na Chama cha Kongresi ya Wananchi na waitifaki wake.