Al Kadhimi: Iraq haiwahitaji wanajeshi wa Marekani
https://parstoday.ir/sw/news/west_asia-i72772-al_kadhimi_iraq_haiwahitaji_wanajeshi_wa_marekani
Waziri Mkuu wa Iraq amesema kuwa Baghdad haiwahitaji wanajeshi wa Marekani kwa ajili ya kupambana na kundi la Daesh.
(last modified 2025-11-07T02:31:33+00:00 )
Jul 26, 2021 02:38 UTC
  • Mustafa Al-Kadhimi
    Mustafa Al-Kadhimi

Waziri Mkuu wa Iraq amesema kuwa Baghdad haiwahitaji wanajeshi wa Marekani kwa ajili ya kupambana na kundi la Daesh.

Bila ya kuainisha muda maalimu wa kuondoka wanajeshi wa Marekani nchini Iraq, Mustafa Al-Kadhimi ambaye ameelekea Marekani, amesema fremu rasmi ya kupelekwa tena askari wa Marekani nchini humo inategemea matokeo ya mazungumzo yake na viongozi wa serikali ya Washington. Akijibu swali kuhusu uwezekano wa kubadilishwa  majukumu ya wanajeshi wa Marekani huko Iraq, Al Kadhimi amesema: Baghdad itaiomba Marekani msaada wa ushirikiano kwa ajili ya kutoa mafunzo na kukusanya taarifa za kijeshi. 

Wanajeshi vamizi wa Marekani huko Iraq 

Waziri Mkuu wa Iraq amesema kuwa, vikosi vya usalama na jeshi la Iraq vina uwezo wa kuilinda nchi hiyo bila ya msaada wa wanajeshi wa muungano unaoongozwa na Marekani.

Ripoti zinasema kuwa, Waziri Mkuu wa Iraq Mustafa al Kadhimi leo Jumatatu atakuwa na mazungumzo na Rais Joe Biden wa Marekani kuhusu masuala ya kistratejia.  

Leo Jumatatu Biden na al Kadhimi watajaribu kuainisha jedwali la majukumu ya majeshi ya Marekani huko Iraq.