Dec 31, 2016 08:04 UTC
  • Kumi wauawa kwa risasi katika maeneo tofauti ya Marekani

Polisi ya Marekani imetangaza habari ya kuuawa hivi karibuni watu kumi katika maeeo tofauti ya nchi hiyo

Polisi hiyo imesema watu wengine 7 wamejeruhiwa katika matukio hayo ya ufyatuaji risasi katika pembe tofauti za nchi hiyo. Kwa mujibu wa ripoti ya polisi hiyo, ufyatuaji risasi huo ulitokea katika majimbo ya North Carolina,Tennessee, mji wa Chicago katika jimbo la Illinois, Sacramento katika jimbo la California, Phoenix katika jimbo la Arizona, Frankfort katika jimbo la Kentucky, Trenton katika jimbo la New Jersey mji wa San Francisco mji wa Belle Glade katika jimbo la Florida na katika mji wa San Antonio katika jimbo la Texas.

Ufyatuaji risasi mjini Florida, Marekani

Kwa mujibu wa ripoti ya Kituo cha Twakwimu za Ufyatuaji Risasi cha Marekani, kesi 57,371 za ufyatuaji risasi zimeripotiwa tokea mwanzo wa mwaka huu hadi kufikia tarehe 9 mwezi huu wa Disemba ambapo watu 859,000 wameuawa na wengine 315,000 kujeruhiwa.

Tags