UN: Wakimbizi Waislamu wa Rohingya wanakabiliwa na hatari kubwa
Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa una wasiwasi kuhusu hatari zinazowakabili Waislamu wakimbizi wa Rohingya katika wimbi la kufukuzwa huko Myanmar.
Msemaji wa Kamisheni Kuu ya Wakimbizi ya Umoja wa Mataifa (UNHCR), William Spindler amesema kuwa kamisheni hiyo ina wasiwasi mkubwa kufuatia ongezeko la idadi ya Waislamu hao ambao wanatumia njia hatari wakikimbia ukatili na mauaji nchini Myanmar.
Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa tangu mwezi Agosti hadi sasa Waislamu wa jamii ya Rohingya zaidi ya 200 ambao walikuwa na lengo la kufika nchini Bangladesh kupitia mpaka wa majini wa mto Naf kati ya nchi hiyo na Myanmar, wameghiriki na kufariki dunia.
Msemaji wa UNHCR ameongeza kuwa, wakimbizi waliodhulumika wa Myanmar hawana fedha wala suhula zinazohitajika na hivyo wanalazimika kutumia vifaa hatari kama magogo ya miti yanayoelea ili kuwavusha katika njia hiyo ya majini ya mpakani kati ya Myanmar na Bangladesh, hatua ambayo inasababisha ajali nyingi za kughariki baharini.