UNHCR, UNDP zataka Myanmar iandae mazingira ya kurejea Waislamu Warohingya
https://parstoday.ir/sw/news/world-i47320-unhcr_undp_zataka_myanmar_iandae_mazingira_ya_kurejea_waislamu_warohingya
Mashirika ya misaada ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa yameitaka serikali ya Myanmar iandae mazingira ya kurejea katika jimbo la Rakhine Waislamu Warohingya wa nchi hiyo.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Aug 08, 2018 23:54 UTC
  • UNHCR, UNDP zataka Myanmar iandae mazingira ya kurejea Waislamu Warohingya

Mashirika ya misaada ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa yameitaka serikali ya Myanmar iandae mazingira ya kurejea katika jimbo la Rakhine Waislamu Warohingya wa nchi hiyo.

Taarifa ya mashirika hayo imeeleza kuwa, serikali ya Myanmar inapaswa kuandaa mazingira ya kurejea nchini humo Waislamu wa kabila la Rohingya waliokimbilia nchi jirani ya Bangladesh.

Taarifa ya pamoja ya Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP) imeeleza kwamba, mashirika hayo yanahitajia kuwafikia Waislamu wa jamii ya Rohingya katika jimbo la Rakhine na kwamba, yanasubiri idhini tu ya kupelekwa vikosi vya kimataifa katika mji wa Maungdaw ulioko katika jimbo hilo.

Waislamu Warohingya wakikimbia makazi yao ili kukwepa mauaji ya jeshi na mabudha dhidi yao

Hadi sasa viongozi wa serikali ya Myanmar hawajatoa jibu lolote kuhusiana na takwa hilo na mashirikak ya UNHCR na UNDP.

Juni 14 mwaka huu, Umoja wa Mataifa ulitiliana saini makubaliano na serikali ya Myanmar ambapo lengo la makubaliano hayo lilikuwa ni kuruhusu mamia ya wakimbizi wa jamii ya Rohingya walioko Bangladesh warejee katika jimbo la Rakhine ambalo kimsingi ndiyo makazi yao ya asili.

Wimbi jipya la jinai dhidi ya Waislamu Wararohingya zilishika kasi tangu tarehe 25 mwezi Agosti mwaka jana. Hadi sasa  jinai hizo zimepelekea kuuliwa Waislamu karibu elfu 10 na kujeruhiwa makumi ya maelfu ya wengine huku wengine karibu laki nane wakilazimika kuwa wakimbizi katika nchi jirani ya Bangladesh.