Mar 12, 2017 16:29
Amani ya Allah, rehma na baraka zake ziwe juu yenu wapenzi wasikilizaji. Karibuni kusikiliza kipindi hiki kinachozungumzia suala muhimu na la msingi, la umoja katika Ulimwengu wa Kiislamu. Suala ambalo kutokana na kipindi ambacho Ulimwengu wa Kiislamu unakipitia hivi sasa, umuhimu wake unahisika zaidi wakati huu, pengine kuliko wakati mwengine wowote ule. Endeleeni basi kuwa pamoja nami kuanzia awali hadi tamati ya mfululizo huu, hii ikiwa ni sehemu yake ya tatu.