Feb 19, 2024 11:08
Utawala wa Kizayuni wa Israel umeidhinisha mpango wa kuwawekea vizuizi vikali Wapalestina wanaoishi kwenye ardhi zilizoanza kukaliwa kwa mabavu mwaka 1948 na wa mji wa Baitul Muqaddas (Jeruselem) vya kuingia kwenye Msikiti wa Al Aqsa wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani, utakaoanza wiki ya pili ya mwezi ujao wa Machi.