-
Odinga kwenda Mahakama ya Juu Kenya kupinga matokeo ya urais
Aug 16, 2017 11:18Kinara wa muungano wa upinzani wa NASA nchini Kenya, Raila Odinga hatimaye amepasua mbarika na kusema kuwa ataenda katika Mahakama ya Juu ya nchi kupinga matokeo ya kura za urais yaliyompa ushindi Rais Uhuru Kenyatta wa chama cha Jubilee.
-
Polisi yashutumiwa kwa kuvamia ofisi za asasi zisizo za serikali Kenya
Aug 16, 2017 09:57Mashirika ya kiraia na yale ya kutetea haki za binadamu yamekosoa vikali hatua ya vyombo vya dola ya kuvamia na kutaka kufunga kwa nguvu ofisi ya asasi isizo ya serikali katika mji mkuu Nairobi.
-
Odinga: Kesho Jumatatu msiende kazini, Jumanne nitatoa tangazo muhimu
Aug 13, 2017 09:18Kinara wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga amewataka wafuasi wake wasiende kazini kesho Jumatatu na wajiandae kupokea kile alichokitaja kuwa maelekezo na tangazo zito litakalotikisa taifa siku ya Jumanne.
-
Ushindi wa Uhuru Kenyatta katika uchaguzi wa Rais nchini Kenya
Aug 12, 2017 03:54Hatimaye na baada ya mjadala mkubwa kuhusu matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 8 Agosti, Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya (IEBC) jana usiku ilimtangaza Uhuru Kenyatta kuwa ndiye aliyeibuka na ushindi wa kiti cha rais wa nchi hiyo.
-
NASA: Tutakubali matokeo ya uchaguzi kwa masharti
Aug 11, 2017 12:38Muungano wa upinzani wa NASA nchini Kenya umetangaza kuwa utakubali matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika juzi kote nchini humo iwapo utaruhusiwa kutazama data za asili katika sava za kumputa za Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya nchi hiyo (IEBC).
-
EU yazitaka pande zote kuheshimu sheria nchini Kenya
Aug 11, 2017 11:23Umoja wa Ulaya umetangaza kuwa unafuatilia kwa makini mwenendo wa uchaguzi wa hivi karibuni huko Kenya.
-
Taharuki Kenya huku matokeo ya uchaguzi wa urais yakisubiriwa kwa hamu
Aug 11, 2017 03:15Hali ya taharuki imetanda nchini Kenya huku Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka nchini humo (IEBC) ikitazamiwa kumtangaza mshindi wa uchaguzi wa urais wakati wowote tokeo sasa hii leo.
-
Upinzani Kenya waitaka IEBC imtangaze Raila Odinga mshindi wa uchaguzi wa urais
Aug 10, 2017 10:47Mrengo wa upinzani wa NASA nchini Kenya umeitaka Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka IEBC imtangaze mgombea wa muungano huo Raila Odinga kuwa, mshindi wa uchaguzi wa urais uliofanyika nchini humo siku ya Jumanne.
-
Watu 5 wameuawa katika ghasia za baada ya uchaguzi mkuu Kenya
Aug 10, 2017 04:18Watu 5 wameripotiwa kuuawa katika ghasia na machafuko ya baada ya uchaguzi mkuu uliofanyika juzi nchini Kenya baada ya kinara wa kambi ya upinzani, Raila Odinga kudai kuwa kumefanyika udanganyifu mkubwa.
-
Igad: Uchaguzi mkuu Kenya umefanyika kwa amani, uwazi na utaratibu sahihi
Aug 09, 2017 11:41Timu ya wasimamizi wa uchaguzi ya Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiserikali wa Nchi za Mashariki na Pembe ya Afrika (Igad) imeipongeza Tume Huru ya Uchaguzi ya Kenya (IEBC) kwa kusimamia uchaguzi kwa njia sahihi na kusema kuwa, tume hiyo inapaswa kuwa kigezo cha kuigwa na nchi nyingine za Afrika.