-
Rais wa Equitorial Guinea ahifadhi kiti chake kwa kupata 98% ya kura
Apr 26, 2016 03:53Matokeo ya awali ya uchaguzi mkuu nchini Equitorial Guinea yanaonyesha kuwa Rais Teodoro Obiang Nguema ameshinda kiti hicho kwa kupata asilimia 98 ya kura zilizopigwa.
-
Wapinzani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wataka kufanyika uchaguzi mkuu wa nchi hiyo Novemba mwaka huu
Apr 25, 2016 02:25Wapinzani wa serikali katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wametoa wito wa kufanyika uchaguzi mkuu wa nchi hiyo Novemba mwaka huu kama ilivyokuwa imepangwa hapo awali.
-
AU: Uchaguzi wa Djibouti ulikuwa huru na wa haki
Apr 11, 2016 03:33Licha ya lalama kutoka vyama vya upinzani, lakini Umoja wa Afrika AU umesema uchaguzi mkuu wa Djibouti wa Ijumaa iliyopita ulikuwa huru na wa haki.
-
Upinzani Djibouti: Kulikuwa na udanganyifu kwenye uchaguzi wa rais
Apr 10, 2016 03:21Viongozi wa upinzani nchini Djibouti wametangaza kutotambua ushindi wa Rais Ismail Omar Guelleh katika uchaguzi mkuu uliofanyika Ijumaa iliyopita.
-
Uchaguzi wa rais Djibouti, baadhi ya wakuu wa upinzani waususia
Apr 08, 2016 04:36Wananchi wa Djibouti waliotimiza mashari ya kupiga kura leo wameelekea kwenye masanduku ya kupiga kura kumchagua rais mpya, katika uchaguzi ambao aghalabu ya vyama vya upinzani nchini humo vimeususia.
-
Mahakama ya Juu Uganda yatupilia mbali kesi ya kupinga ushindi wa Museveni
Mar 31, 2016 09:33Mahakama ya Juu ya Uganda imetupilia mbali kesi iliyowasilishwa na Waziri Mkuu wa zamani nchini humo Amama Mbabazi ya kupinga ushindi wa Rais Yoweri Museveni katika uchaguzi wa rais wa Februari mwaka huu.
-
UN yasisitiza udharura wa kufanyika mazungumzo DRC
Mar 24, 2016 03:38Mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo amesema kuna udharura wa kufanyika mazungumzo baina ya wanasiasa wa nchi hiyo kwa shabaha ya kukomesha hitilafu za ndani.
-
Mgombea mwingine wa rais Marekani afuata nyayo za Trump
Mar 23, 2016 02:57Mgombea wa kiti cha rais kupitia chama cha Republican Ted Cruz amependekeza kuazishwa msako mkali dhidi ya wafuasi wa dini ya Kiislamu eti kwa shabaha ya kuwazuia ‘wasiingie kwenye kundi la wenye misimamo iliyofurutu ada’.
-
Shein ashinda uchaguzi wa rais Zanzibar kwa 91%, Maalim Seif 1.9% licha ya kususia
Mar 21, 2016 11:45Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC imemtangaza mgombea wa kiti cha rais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM, Dakta Ali Muhammed Shein kuwa mshindi wa uchaguzi wa marudio uliofanyika jana visiwani humo.
-
Chaguzi sita zafanyika Afrika leo
Mar 20, 2016 12:39Leo kumekuwa na upigaji kurakatika nchi sita za Afrika yaani nchini Kongo Brazzaville, Benin, Niger, Cape Verde, Visiwani Zanzibar nchini Tanzania na kura ya maoni nchini Senegal.