-
Johnson: Tutaendelea kufanya mazungumzo na Taliban
Aug 28, 2021 08:11Waziri Mkuu wa Uingereza amesema hakuna uhusiano wowote kati ya Daesh na Taliban na kueleza kuwa serikali ya Uingereza itaendelea kufanya mazungumzo na kundi la Taliban.
-
Matukio ya Afghanistan; sisitizo la umuhimu wa muqawama katika eneo la Asia Magharibi
Aug 28, 2021 02:37Matukio ya majuma mawili ya hivi karibuni nchini Afghanistan yameonyesha kuwa, makundi ya mapambano na muqawama katika eneo la Asia Magharibi yana nafasi muhimu katika kulinda mamlaka ya kujitawala pamoja na usalama wa mataifa yao.
-
Safari ya Shah Mahmood Qureshi mjini Tehran; Afghanistan ajenga kuu ya mazungumzo ya Iran na Pakistan
Aug 27, 2021 13:20Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Pakistan amekutana na kufanya mazungumzo hapa mjini Tehran na Rais Ibrahim Raeisi na kujadili pamoja na kubadilishana mawazo kuhusiana na uhusiano wa pande mbili huku matukio ya hivi karibuni nchini Afghanistan yakitawala katika mazungumzo yao.
-
Iran yalaani mashambulio ya Kabul, ISIS yatangaza kuhusika nayo
Aug 27, 2021 08:09Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani vikali mashambulio ya kigaidi yaliyotokea nje ya uwanja wa ndege wa Kabul nchini Afghanistan jana Alkhamisi.
-
Merkel aitaka jamii ya kimataifa kuzungumza na Taliban
Aug 26, 2021 03:44Kinyume kabisa na msimamo wa Umoja wa Ulaya kuhusu kundi la wanamgambo wa Taliban la Afghanistan, Kansela wa Ujerumani Angela Merkel ameitolea mwito jamii ya kimataifa kufanya mazungumzo na kundi hilo.
-
Wakimbizi kutoka Afghanistan waanza kuwasili Uganda
Aug 25, 2021 12:57Kundi la kwanza la makumi ya wakimbizi kutoka Afghanistan limewasili nchini Uganda.
-
Taliban: Hatutaongeza muda wa siku ya mwisho ya askari wa kigeni kuondoka Afghanistan
Aug 24, 2021 02:47Taliban imetoa onyo kwa Marekani ikisisitiza kuwa, siku ya mwisho iliyoainishwa kwa askari wa nchi hiyo kuondoka Afghanistan ni "mstari mwekundu" kwa kundi hilo na kwamba kurefushwa kwa muda wa zoezi hilo kutakuwa na "matokeo mabaya".
-
Askari wa Marekani wawalaghai Waafghani wanaotaka kuondoka Kabul
Aug 23, 2021 03:31Imefichuka kuwa, maafisa usalama wa Marekani walioko katika Uwanja wa Ndege wa Kabul nchini Afghanistan wanawaitisha mlungula Waafghani wanaotaka kuondoka katika mji mkuu huo.
-
Kupinga Putin ombi la Biden la kuasisi kituo cha kijeshi karibu na Afghanistan
Aug 21, 2021 10:12Gazeti linalochapishwa nchini Marekani la Wall Street Journal limeandika kuwa, Rais Vladimir Putin wa Russia katka mazungumzo ya tarehe 16 Juni aliyofanya na Rais wa Marekani amepinga ombi la Biden la kutaka Washington kuwa na nafasi yoyote katika nchi za Asia ya Kati.
-
Washington Examiner: Joe Biden anakimbia Afghanistan
Aug 21, 2021 07:12Mtandao wa habari wa Washington Examiner umejadili kadhia ya Afghanistan kwa makala yenye kichwa cha habari: "Joe Biden anakimbia Afghanistan" na kusema, Marekani imejidanganya na kuona ndoto huko Afghanistan.