-
Sisitizo la Kiongozi Muadhamu la uungaji mkono wa Iran kwa wananchi wa Afghanistan
Aug 29, 2021 05:16Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu sambamba na kuashiria mazingira ya sasa ya Afghanistan amesisitiza himaya na uungaji mkono wa Jamhuri ya Kiislamuu ya Iran kwa wananchi wa nchi hiyo.
-
Baqeri: Marekani imeondoka Afghanistan baada ya kushindwa kwa fedheha
Aug 29, 2021 03:09Mkuu wa Kamandi ya Majeshi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, Marekani imeondoka nchini Afghanistan baada ya kushindwa kwa fedheha.
-
Johnson: Tutaendelea kufanya mazungumzo na Taliban
Aug 28, 2021 03:41Waziri Mkuu wa Uingereza amesema hakuna uhusiano wowote kati ya Daesh na Taliban na kueleza kuwa serikali ya Uingereza itaendelea kufanya mazungumzo na kundi la Taliban.
-
Matukio ya Afghanistan; sisitizo la umuhimu wa muqawama katika eneo la Asia Magharibi
Aug 27, 2021 22:07Matukio ya majuma mawili ya hivi karibuni nchini Afghanistan yameonyesha kuwa, makundi ya mapambano na muqawama katika eneo la Asia Magharibi yana nafasi muhimu katika kulinda mamlaka ya kujitawala pamoja na usalama wa mataifa yao.
-
Safari ya Shah Mahmood Qureshi mjini Tehran; Afghanistan ajenga kuu ya mazungumzo ya Iran na Pakistan
Aug 27, 2021 08:50Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Pakistan amekutana na kufanya mazungumzo hapa mjini Tehran na Rais Ibrahim Raeisi na kujadili pamoja na kubadilishana mawazo kuhusiana na uhusiano wa pande mbili huku matukio ya hivi karibuni nchini Afghanistan yakitawala katika mazungumzo yao.
-
Iran yalaani mashambulio ya Kabul, ISIS yatangaza kuhusika nayo
Aug 27, 2021 03:39Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani vikali mashambulio ya kigaidi yaliyotokea nje ya uwanja wa ndege wa Kabul nchini Afghanistan jana Alkhamisi.
-
Merkel aitaka jamii ya kimataifa kuzungumza na Taliban
Aug 25, 2021 23:14Kinyume kabisa na msimamo wa Umoja wa Ulaya kuhusu kundi la wanamgambo wa Taliban la Afghanistan, Kansela wa Ujerumani Angela Merkel ameitolea mwito jamii ya kimataifa kufanya mazungumzo na kundi hilo.
-
Wakimbizi kutoka Afghanistan waanza kuwasili Uganda
Aug 25, 2021 08:27Kundi la kwanza la makumi ya wakimbizi kutoka Afghanistan limewasili nchini Uganda.
-
Taliban: Hatutaongeza muda wa siku ya mwisho ya askari wa kigeni kuondoka Afghanistan
Aug 23, 2021 22:17Taliban imetoa onyo kwa Marekani ikisisitiza kuwa, siku ya mwisho iliyoainishwa kwa askari wa nchi hiyo kuondoka Afghanistan ni "mstari mwekundu" kwa kundi hilo na kwamba kurefushwa kwa muda wa zoezi hilo kutakuwa na "matokeo mabaya".
-
Askari wa Marekani wawalaghai Waafghani wanaotaka kuondoka Kabul
Aug 22, 2021 23:01Imefichuka kuwa, maafisa usalama wa Marekani walioko katika Uwanja wa Ndege wa Kabul nchini Afghanistan wanawaitisha mlungula Waafghani wanaotaka kuondoka katika mji mkuu huo.